Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, May 12, 2016

AFISA MFAWIDHI WA SUMATRA MKOA WA NJOMBE JOSEPH BURONGO AFUNGA MAFUNZO YA UDEREVA UTARINGORO NJOMBE




 MADEREVA WA BODABODA WA KATA YA UTARINGORO WAKIWA KWENYE MAANDAMANO  WAKATI WA KUFUNGA MAFUNZO HAYO

 WA UPANDE WA KULIA NI AFISA MFAWIDHI WA SUMATRA MKOA WA NJOMBE JOSEPH BURONGO,WA PILI KUTOKA KULIA  NI MRATIBU WA FUTURE WORLD  VOCATION CENTRE  KUTOKA DAR ES SALAAM YUSTO WALISIMBA MKOLA NA WA TATU NI AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA UTARINGORO ISABELA MALANGALILA NAYE MIONGONI MWA WAHITIMU WA MAFUNZO YA UDEREVA.




 AFISA USALAAMA WA BARABARANI MKOA WA NJOMBE SANJENT BRAISON KAMBO AKITOA ELIMU JUU YA MAFUNZO WALIOPEWA MADEREVA HAO NA SHERIA ZAKE




 AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA UTARINGORO ISABELA MALANGALILA AKISOMA LISARA YA WAHITIMU WA MAFUNZO YA UDEREVA AKIWEMO YEYE MWENYEWE NAYE KAPATIWA MAFUNZO HAYO
 AFISA MFAWIDHI WA SUMATRA MKOA WA NJOMBE  JOSEPH BURONGO AKIZUNGUMZA NA WAHITIMU WA MAFUNZO YA UDEREVA UTARINGORO






Serikali  Mkoani Njombe Imewataka Wamiliki Na Madereva  Wa Vyombo Vya Moto  Kuwa  Wavumilivu  Wakati Juhudi Za Kusogeza Huduma  Mbalimbali  Zikifanyika  Ikiwemo  Zoezi La Kutoa Leseni Kwa Waliopatiwa Mafunzo Ya Udereva Ambapo  Ifikapo Mwezi Julai Mwaka Huu Leseni Za Udereva Zitakuwa Zinatolewa Mkoani Njombe.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Afisa Mfawidhi Wa Mamlaka Ya Udhibiti Wa Usafiri Wa Nchi Kavu Na Majini Mkoa Wa  Njombe Sumatra Joseph Burongo Wakati Akifunga Mafunzo Ya Udereva   Kwa  Wahitimu Wa Mafunzo Hayo Katika Kijiji Cha Utaringoro Yaliyodumu Kwa Takribani Siku Saba Yakitolewa Na Wakufunzi Wa Kutoka Future World Vocation  Centre   Kutoka Jijini Dar Es Salaamu.

Burongo Amesema  Mpango Wa Serikali  Mkoa Wa Njombe Ni Kusogeza Huduma Karibu Na Wananchi   Ambapo Kwa Upande Wa Madereva    Wataendelea Kufuatilia Leseni Hizo Kwenye Mikoa Ya Luvuma,Mbeya Na Iringa    Ambapo Amesema  Kwa Wamiliki Wa Pikipiki Na Pikipiki Za Magurudumu Matatu Maarufu Bajaji  Leseni Za Sumatra Wanachukulia Halmashauri  Na Miji Husika.

Awali Akizungumza  Afisa Usalaama Wa Barabarani  Mkoa Wa Njombe Sajent Braison Kambo  Ametaka Wahitimu Wa Mafunzo Hayo  Wanatakiwa Kuzingatia Elimu Waliyoipata Kutoka Kwa Wakufunzi Hao  Kwa Kwa Kuepukana Na Matukio Ya Ajali  Huku Akitaka Kushawishi Madereva Wengine Wasiyo Na Leseni  Wakiwemo Akina Mama  Ili Kupunguza Vifo Vitokanavyo Na Ajali Za Barabarani.

Mratibu Wa Taasisi Ya Future World  Vocation  Trainning  Centre Kutoka Jijini Dar Es Salaamu  Yusto  Walisimba  Mkola  Ametaka  Wahitimu Hao Kulipia Bima Za Pikipiki  Na Vyombo Vyao Vya Moto Kwa Manufaa Yao   Huku Akisema Leseni Haiwezi Kuzuia Ajali Isipokuwa Ni Umakini  Na Kuzingatia Alama Za Barabarani Ambacho Wamesisitiza Wakati Wa Utoaji Wa Mafunzo.

Isabela Malangalila Ni Miongoni Mwa Wahitimu Wa Mafunzo Hayo   Akisoma Taarifa Fupi Kwa Niaba Ya Wahitimu Wote Ametaja Changamoto Mbalimbali Zinazowakabili Madereva Wa Vyombo Vya Moto  Zikiwemo Za Kufuata Leseni Na Huduma Nyingine Kutoka Nje Ya Mkoa Wa Njombe.

Kwa Upande Wake Wahitimu Wa Mafunzo Hayo Wamepongeza  Taasisi Ya The Future World Vocation Centre Kwa Kuwapatia Mafunzo Hayo Na Kuelezea Namna  Watakavyo  Nufaika  Kwani Wameahidi Kuitumia Elimu Waliyo Ipata Ipasavyo  Na Kuwashawishi Madereva Wengine Kujiunga  Na Mafunzo Ili Kuepukana Na Usumbufu Wa  Kusimamishwa Na Kutozwa Faini Na Maafisa Usalaama Wa Barabarani.

No comments:

Post a Comment