Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, May 9, 2016

TASAF NJOMBE YAWANUFAISHA WANANCHI WA KAYA MASIKINI,WENGINE WAO WATUMIA KWENYE KILIMO CHA MIWA,MANANASI NA UFUGAJI

 BAADHI YA WAKAZI WA BWILAYA YA NJOMBE AMBAO NI WANUFAIKA WA MPANGO WA  TASAF

 HAWA NI WAZEE WA KATA YA KIDEGEMBYE NAO WANUFAIKA NA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI  TASAF  SASA WATAKA SERIKALI IFIKILIA MATIBABU BURE KWA WAZEE NA PENSHEN


 WAKATI WAKIWA KWENYE ZOEZI LA KUPOKEA FEDHA HIZO
 WANUFAIKA HAO WAKISHAPEWA FEDHA HIZO ZINAWANUFAISHA KATIKA SWALA LA MATIBABU NA HAPA NI ZAHANATI AMBAYO IPO KWA MANUFAA YA WAKAZI HAO



 MANANASI NAYO NI MIONGOZI MWA KILIMO WANACHOJIKITA KULIMA




MASHAMBA YA MIWA NAYO  YAHUSIKA KATIKA KILIMO KWA WANUFAIKA WA MPANGO WA TASAF


Wakulima Wa Zao La Matunda Ya Mananasi  Waliopo Katika Kijiji Cha Madeke Wilayani Njombe Wameiomba  Serikali  Mkoani Hapa   Kuwatafutia Soko La Uhakika Kwaajili Ya Kuuza  Matunda Wanayozarisha Aina Ya Mananasi Na Maparachichi  Ili Kuongeza Uchumi  Wa Halmashauri  Na Wakulima  Hao Kwani Kwa Sasa Wanakabiliwa Na Kuoza Kwa Matunda Hayo.

Wakizungumza Na Uplands Fm  Baadhi Ya Wananchi Wa Kijiji Cha Madeke  Wamepongeza Mtaalamu Wa Kilimo Kata Na Kijiji  Hicho Kwa Kuhamasisha  Wananchi Kutumia Kilimo Hai  Katika Kilimo Cha Mananasi Na Mazao Mbalimbali Yanayostawi Pasipo Kutumia Mbolea Za Chumvichumvi  Ambapo Pamoja Na Kilimo Hicho Lakini Bado Changamoto Ya Soko La Kuuzia Matunda Hayo Ni Changamoto Kwao.

Aidha Wananchi Hao Wamesema Vifaa Vya Mashine Ya Kusindika Mananasi Katika Kijiji Hicho Tangu Ipelekwe Na Halmashauri   Ina Takribani Zaidi Ya Miaka Mitatu Mashine Haifanyi  Kazi  Ikiwa Wakulima  Wameongeza Kilimo Cha Manansi  Kutoka Kwenye Ekari Moja Hadi Ekari Sita Kwa Mkulima Mmoja  Ambapo Changamoto Kubwa Matunda Hayo Yanaozea Mashambani Kwa Kukosa Soko.

Hata Hivyo Wananchi Hao Wamesema  Kinachochangia Kwa Kiasi Kikubwa Kukosa Hata Soko La Ndani Ya Mkoa Wa Njombe Na Mkoa Jirani Wa Morogoro Ni Uwepo Wa Miundombinu Mibovu Ya Barabara  Ambazo Hazipitiki Kwa Msimu  Wa Mvua  Na Kusababisha Magari Kikwama Na Kulaza Mizingo Polini Jambo Ambalo Wamiliki Wa Magari Hawataki Kupeleka Magari Yao Huko.

Akizungumza Kwa Upande Wake Mwenyekiti Wa Serikali Ya Kijiji Cha Madeke Dikray Kyerula  Amekili Kuwepo Kwa Changamoto Ya Wakulima Wa Kilimo Hai Kukabiliwa Na Tatizo La Kukosekana Kwa Soko La Matunda Licha Ya  Halmashauri Kuweka Mikakati Ya Kupeleka Mashine Ya Kusindika Matunda  Huku Akisema Matunda  Mengi Yanaozea Shambani Kwa Kukosa Wateja.

Akizungumzia Kilimo Hai Kinavyoweza Kuwanufaisha Wakulima Wa Matunda Katika Kijiji Cha Madeke Afisa Kilimo  Na Mifugo Onesmo Mfugale  Amesema Serikali Iko Mbioni Kulitafutia Ufumbuzi Tatizo La Soko Kwa Kukamilisha Miundombinu Ya Kiwanda Cha Kusindika Mananasi Na Matunda Mengine Kama Maparachichi Na Matunda Mengine Huku Akisisitiza Wananchi Kutumia Kilimo Hai Kupata Soko Zaidi.

Kwa Upande Wake Diwani Wa Kata Ya Mfriga Vasco Mgunda Amesema Serikali Inaendelea Na Jitihada Za Kutatua Changamoto Ya Miundombinu  Ya Barabara  Zinazoelekea  Kwenye Kata Hiyo  Za Kuwatafuta Wadau Mbalimbali Wa Kununua Matunda Katika Kata Ya Mfriga  Ambapo Kuhusu Kiwanda Cha Kusindika Matunda Amesema  Bado Hajafuatilia Kujua Tatizo Lake Na Kuahidi Kufatilia Halmashauri Kufahamu Kinachokwamisha Kuanza Kufanya Kazi.

No comments:

Post a Comment