Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, January 12, 2016

WANANCHI WATAKIWA KUFUGA NYUKI NA KUPANDA MITI YA MATUNDA AINA YA PARACHICHI


 MKURUGENZI   WA SHIRIKA LA FORE STERING ECONOMIC ATUKUZWE MWENDAMSEKE
Shirika La Fore Stering Economy Linalojihusisha Na Utunzaji Wa Mazingira  Mkoani Njombe Limewataka Wananchi Kutunza Mazingira Kwa Kupanda Miti Yenye Maua Kwaajili Ya Chakula  Cha Wadudu Wa Porini Hususani Nyuki  Pamoja Na Wananchi Hao Kuhusika Na Utengenezaji Wa Mizinga Kwaajili Ya Kufunga Nyuki.

Akizungumza Na  Mtandao Huu Mkurugenzi Wa Shirika Hilo  Atukuzwe Mwendamseke  Amesema Shirika La Fore Stering Economy  Pia Linatoa Elimu Ya Ujasiliamali Na Elimu Ya Kujitegemea Kwa Kujiajiri Kwa Baadhi Ya Vijana Ambao Wanatoka Vyuoni Na Shuleni  Na Kusaidia Kuondoa Utegemezi Wa Kupatiwa Ajira Serikalini Badala Yake Wajiajiri.

 Aidha Mwendamseke Amesema Shirika Hilo Limejipanga Kutoa Elimu Ya Uhifadhi Na Namna Ya Kulina Asali Kwa Njia Ya Kisasa Kwa Wafugaji Wa Nyuki   Ili Wapate Soko  La Asali Nchini  Na Nje Ya Nchi  Ambapo Amesema Kwa Anayehitaji Kufuga  Wadudu Hao Anapaswa Kupanda Hata Miti Ya Miparachichi  Ambayo Itawapatia Faida Mara Dufu.

Mwendamseke Amepongeza Wananchi Wa Wilaya Ya Ludewa Kwa Kuongeza Jitihada Za  Kufuga Nyuki Licha  Yakuwepo Kwa Changamoto Ndogo Ya Kuhifadhi Asali Na Nnta Na Kwamba Kuna Kampuni Ya Manongo Imeanza Kukusanya Asali Na Nnta  Zinazopatikana Kwa Wafugaji Wa Nyuki Mkoani Njombe.

Kwa Upande Wake Baadhi Ya Wafugaji Wa Kutoka Lupembe  Na Baadhi Ya Maeneo Ya Ludewa Wameomba Elimu Kutolewa Kwa Wingi Kwa Wafugaji Hao Wa Nyuki  Kwa Kushirikiana Na Serikali  Ili Kufanikisha Zoezi La Ufugaji Huo Kuliko Kuliachia Shirika Peke Yake Kutoa Elimu Hiyo.

No comments:

Post a Comment