Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, January 12, 2016

VYOMBO VYA MOTO VYA TAKIWA KUFUATA SHERIA ,KANUNI NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI



 AFISA USALAMA WA BARABARANI HAPPY ROSE AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI AKIWA KATIKA OFISI ZA UPLANDS RADIO NJOMBE
 MKAGUZI WA MAGARI NMKOA WA NJOMBE  COPLO WILLIAM  KATIKA PICHA

Jeshi La Polisi Mkoani Njombe Limewataka Watumiaji Wa Vyombo Vya Moto Kufuata Kanuni Na Sheria Za Usalama Barabarani Ili Kuepusha Ajali Na Kwamba Jeshi La Polisi Limejipanga Kukomesha Tabia Za Kuendesha  Vyombo Vya Moto Kwa Kasi .

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Afisa Usalama  Barabarani  Happy Rose  Amesema Jeshi La Polisi Limekuwa Likitoa Elimu Ya Usalaama Barabarani Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Mkoa Wa Njombe Pamoja Na Kuwakumbusha Madereva Juu Ya Alama za Usalama Barabarani Ili Kupunguza Ajari Hizo.

Aidha  Rose Amesema Chanzo Kikubwa Cha Ajali Hizo Kinatokana na Baadhi ya Madereva Wengi Kutumia Vibaya  Vyombo  Vyao  Vya Moto  Na Kwamba Jeshi la Polisi  Linasimamia Sheria Kwa Madereva Wanaokiuka  Sheria  Hizo  Ambapo   Hatua  Mbalimbali  Zimekuwa  Zikichukuliwa  Dhidi  Ya  Wanaokiuka  Kwa Kuwaelimisha  Na Kutaka Waheshimu  Alama Hizo.

Kwa Upande Wake Mkaguzi Wa Magari Mkoa Wa Njombe Coplo William  Amesema Suala La Mwendo Kasi Barabarani Linatakiwa Kuheshimiwa Na Madereva Wote  Wa Vyombo Vya Moto  Wakiwemo Waendesha Pikipiki Na Magari  Na Kutumia Elimu Walizozipata Wakiwa Darasani Kuzitumia  Na Kuzitambua Na Kutafsiri Alama Hizo Kuepusha Ajali.

No comments:

Post a Comment