Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, January 12, 2016

DIWANI WA KATA YA ITULAHUMBA TITO MDENDEMI AZUIA MZEE MGUTE ASIUZE NYUMBA YA WATOTO WAO KATIKA KIJIJI CHA ISINDAGOSI


 DIWANI WA KATA YA ITULAHUMBA BAADA YA KUWASILI KWENYE NYUMBA WANAYOISHI WATOTO  WA MZEE MGUTE AMBAYE ANALALAMIKIWA KUTAKA KUUZA NYUMBA NA MAENEO HUKU WATOTO WAKIWA NDANI NA MAMA YAO ALIKWISHA KUFARIKI  SASA WATOTO WANASEMA WAENDE WAPI.
 WATOTO AMBAO MAMA YAO ALIKWISHA FARIKI PENDO MGUTE ,WAKIWA NA KAKA YAO WENGINE HAPA HAWAPO KWA MAMA ALIYE FARIKI WAKO WANNE  WOTE WAKIKE LAKINI HUYU KAKA YAO NI WA MAMA MWINGINE LAKINI WALIKUWA MTU NA DADA  WALIOLEWA KWA MTU MMOJA HIVYO KAKA HUYU ANAWASAIDIA DADA ZAKE WASIONDOLEWA KWENYE NYUMBA YA MAREHEMU MAMA YAO

 HAWA NI BAADHI TU YA WANANCHI WALIOKOMALIA JAMBO HILO HADI HAPO LILIPOFIKIA KUHAKIKISHA MWENYEKITI NA MZEE MGUTE HAWAUZI NYUMBA HIZO ZA WATOTO
 DIWANI MDENDEMI AKIWA NA WANANCHI PAMOJA NA WATOTO WA MZEE MGUTE

 ENEO LENYEWE WANALOTAKA KUUZA NI HILI LA NYUMBA YA WATOTO HAO

 HUYU NDIYE DIWANI WA KATA YA ITULAHUMBA WILAYANI WANGING'OMBE TITO MDENDEMI
 DIWANI WA KATA YA ITULAHUMBA TITO MDENDEMI AKIHOJIANO JUU YA WATOTO WALIOUZIWA NYUMBA NA  MAENEO NA BABA YAO
 MWENYEKITI WA KIJIJI CHA ISINDAGOSI ZEBEDAYO DEGE AKITOLEA UFAFANUZI JUU YA TUHUMA ZINAZOMKABILI YEYE NA MZEE MGUTE AKIWA OFISINI KWAKE

Diwani Wa Kata Ya Itulahumba Wilayani Wanging'ombe  Mkoani Njombe Tito Mdendemi  Ameagiza Kusimamishwa Kwa Zoezi La Kuuzwa Kwa Nyumba Ya Watoto Wa Mzee  Meck Mgute  Ambaye Ametuhumiwa Kutaka Kuuza Nyumba Na Maeneo Ya Watoto Wake Wanne  Ambao Hawana Mama Yao Wanaoishi Katika Kijiji Cha Isindagosi.

Agizo Hilo Amelitoa Diwani Wa Kata Hiyo  Mdendemi  Baada Ya Kusikiliza  Malalamiko Ya  Majirani Na  Watoto   Wa Mzee Mgute  Ambaye Ni Baba Wa Watoto  Hao  Akishilikiana Na Mwenyekiti Wa Serikali Ya Kijiji  Cha Isindagosi  Kwamba Wameuza Nyumba Na Maeneo Wanayoishi Watoto Wa Mzee Huyo  Na Kuwafukuza Wakaishi Wanakojua Wao.

Mdendemi Amesema  Wakati Akifuatilia  Kwenye Baraza La  Kata Kujiridhisha Kama Watoto Hao Wamefungua Kesi  Ya Kuuzwa Nyumba  Na Eneo La Marehemu Mama Yao Ikiwa  Wao Bado Wanaishi Kwenye Nyumba Hiyo  Wananchi Wa Kijiji Cha Isindagosi Wanapaswa Kumpatia Taarifa Mara Moja Endapo Kuna Watu Wamefika Kuwahamisha Watoto Hao Ili Sheria Ifuate Mkondo Wake.

Wakizungumza Mbele Ya Diwani Wa Kata Ya Itulahumba  Tito Mdendemi,Watoto Wa Mzee Meck Mgute  Wakiongozwa Dada Yao Mkubwa  Pendo Mgute Akishilikiana Na Kaka Yao Ambaye Ni Mtoto Wa Mama Mdogo Wa Familia Hiyo Ben Mgute Wamemueleza Diwani Huyo Kwamba Mwenyekiti Na Baba Yao Meck Mgute Wameshilikiana Kuwafukuza Watoto  Kwenye Nyumba Ya Marehemu Mama Yao Kwa Kuuza Kwa Shilingi Laki Nane.

Mtandao Huu  Umeongozana Na Diwani Wa Kata  Hiyo Tito Mdendemi  Na Kukutana Na Mwenyekiti Wa Serikali Ya Kijiji Cha Isindagosi  Ambaye Analalamikiwa Kushilikiana Na Mzee Mgute Kuwahamisha Watoto Hao  Zebedayo Dege  Amekanusha Kuhusika Na Tuhuma Hizo Huku Akikili Kupokea Taarifa Za Kuuzwa Kwa Eneo Hilo Toka Kwa Mzee Mgute.

Awali Wananchi Wa Kijiji Cha Isindagosi Kata Ya Itulahumba Wakizungumza Na Uplands Fm  Wameutupia Lawama Uongozi Wa Kijiji Hicho  Hususani Mwenyekiti  Kwa Kuhusika Kutumia Madaraka Yake Vibaya  Kuwashawishi Baadhi Ya Wananchi Wauze Maeneo Yao  Ili Pesa Wampatiye Na Yeye Ikiwemo Kusimamia Kuuzwa Kwa Eneo La Familia Ya Watoto Wanne Licha Ya Mwenyekiti Huyo  Kukanusha Malalamiko Hayo.

No comments:

Post a Comment