Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, January 12, 2016

WANANCHI WA KIJIJI CHA IHANGA WALALAMIKIA KUTOZWA MICHANGO YA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA ANNE MAKINDA IKIWA WATOTO WAO HAWASOMESHI KATIKA SHULE HIYO

 


 
 AFISA ELIMU HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE VENANCE MSUNGU AKIKANUSHA HOJA ZA WANANCHI WA KIJIJI CHA IHANGA KUCHANGISHWA MICHANGO HUKU WATOTO WAO HAWASOMI KATIKA SHULE HIYO AMBAYO  WANADAI NI YA KATA


MDAU WA ELIMU  EMILIAN MSIGWA AMESEMA KIMSINGI SHULE HIYO NI YA VIPAJI MAALUMU INACHUKUA WANAFUNZI KUTOKA MAENEO MBALIMBALI LAKINI ANASHANGAZWA KUONA UTARATIBU WA HALMASHAURI KUWACHANGISHA MICHANGO WANANCHI WA ENEO HUSIKA HUKU WAO WATOTO HAWASOMESHI KWENYE SHULE  HIYO


 HUYU NI MIONGONI MWA WALIONYANYASIKE KWA KUPIGWA BAADA YA KUSHINDWA KUCHANGIA MCHANGO WA SHULE HIYO


















Wananchi Wa Vijiji Vya Kata Ya Ihanga Wameilalamikia Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Kwa

Kuwatoza Michango  Ya  Ujenzi Wa Majengo Ya Shule Ya Sekondari Ya Wasichana  Anne

Makinda Ikiwa Watoto Wa Kutoka Kata Hiyo Hawasomi Katika Shule Hiyo   Ambapo

Wamesema Wamekosa Imani  Na Shule Hiyo Kwamba Huenda Wanachangia Shule Ya Mtu

Binafsi.

Wakizungumza Na Mtandao Huu Wananchi Hao Wamesema   Changamoto  Inayowakabili  Ni

Kulazimishwa  Kuchangia Michango Ya  Shilingi Elfu 32 Kwaajili Ya  Ujenzi Wa Vyoo ,

Madarasa  Na Miundombinu Mingine Ya Shule  Huku Wanaoshindwa Kutoa Michango Hiyo

Wanadhalilishwa Kwa Kupelekwa Rokapu Na Kupewa Adhabu Ikiwa  Hawanufaiki Na Shule

Hiyo.

Aidha Wananchi Hao Wamesema  Wamekosa Imani Na Uwepo Wa Shule Ya Sekondari Ya

Wasichana Ya Anne Makinda  Kuitwa Ya  Kata  Na Wananchi Wa Kata Hiyo Kushiliki

Uchangiaji Wa Michango Mbalimbali  Huku Watoto Wao Wakipelekwa Kusoma Shule Ya

Sekondari Ya Kata Ya Kifanya  Licha Ya Kata Yao  Kuwa Na Shule Ya Sekondari Ya Kata.

Wamesema Kuwa Wanafunzi Wanaosoma Katika Shule Ya Sekondari  Ya Wasichana Ya Anne

Makinda  Wanatoka Sehemu Za Mbali  Ambapo Watoto Wa Kata Ya Ihanga  Wanaosoma Shule

Hiyo   Hata 10 Hawafiki  Huku Ada Ikidaiwa Kutoza Zaidi Ya Shilingi Laki Nane Kwa Kila

Mwanafunzi  Jambo Linasababisha Wananchi Hao Kukosa Imani Na Shule Hiyo .

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari  Kwa Niaba Ya Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji

Wa Njombe Ilumineta Mwenda,Afisa Elimu Shule Za Sekondari Venance Msungu

Amekanusha  Madai Yanayotolewa Na Wananchi Hao  Nakwamba Shule Ya Wasichana Ya

Anne Makinda Inachukua Wanafunzi Wa Kutoka Kata Mbalimbali Za Halmashauri Ya Mji  Na

Kipaumbele Ni Kata Ya Ihanga.

Msungu Amesema Shule Ya Sekondari Ya Anne Makinda Inafadhiliwa Na Mashirika

Mbalimbali   Huku Serikali Kuu Inachangia Fedha Kwenye Shule Hiyo  Kwaajili Ya Kutekeleza

Miradi Mbalimbali  Ikiwemo Ujenzi Wa Vyoo  Na Miundombinu Mingine  Ambapo Kuhusu 

Ukubwa Wa Ada Inayotozwa Katika Shule Hiyo Amesema Kila Mwanafunzi Anachangia

Shilingi Elfu 20 Tu.

  Mbali Na Hayo Wananchi  Wa Kijiji  Hicho Pia Wamelalamikia Uongozi Wa Serikali Ya Kijiji

Chao Kwa Kuwanyanyasa Na Kuwadharirisha  Kwa Kuwapatia Adhabu Za Kuwapiga Na

Virugu Na Kuwamwagia Maji  Wakiwa Kwenye Rokapu Kwa Madai  Wameshindwa Kuchangia

Michango Ya  Kijiji Na Shule  Ya Sekondari  Anne Makinda.

Wakizungumza Na Waandishi Wa Habari Baadhi Ya Wananchi Wa Kijiji Cha Ihanga

Wamesema Kuwa  Hatua Ya Uongozi Wa Kijiji Kufumbia Macha  Wajumbe Na Askali Mgambo

Ambao Wamekuwa Wakiwakamata Baadhi Ya Wananchi Na Kuwadhalilisha Kwa Kuchana

Nguo Zao Na Kuwalaza Chumba Kilichomwagiwa Maji Ni Cha Udhalilishaji Kwao.

Aidha  Wananchi Hao Wamesema  Kitendo Cha Askali Mgambo  Wakishirikiana Na Baadhi Ya

Wajumbe Wa Serikali Ya Kijiji Hicho Kuwavua Ngua  Kwenye Ofisi Ya Serikali Ya Kijiji Ni Cha

Udharirishaji  Na Cha Kukiuka Haki Za Binadamu  Jambo Ambalo Limewalazimu Kuiomba 

Serikali Na Wanasheria Mbalimbali Kuwasaidia Kutatua Tatizo Hilo.

Wakijibu Malalamiko Ya Wananchi Wa Kijiji Hicho Ya Kunyanyaswa Na Kudhalilishwa  Kwa

Kuvuliwa Nguo  Wakiwa Rokapu Ndogo Ya Kijiji Hicho Uongozi Wa Kijiji Hicho Akiwemo Afisa

Mtendaji  Adelhard Mlowe  Wamekanusha Kuwafanyia Vitendo Vya Unyanyasaji Wananchi

Wao Na Kusema Kuwa  Wao Hutoa Adhabu Kwa Kufuata Kanuni Na Sheria  Zilizowekwa.

Wamesema  Baadhi Ya Wananchi Wasiyochangia Michango Kwa Wakati Uongozi Hulazimika

Kuwaita Ofisini Na Kufanya Mazungumzo Nao   Lakini Wale Wanaokaidi  Agizo La Serikali  Ya

Kijiji Ndio Wanatumiwa Askali Mgambo Na Baadhi Ya Wajumbe  Lakini  Hawajashuhudia

Kuwepo  Vitendo Vya Unyanyasaji Vinavyofanywa Na Askali Mgambo Wa Kijiji Hicho.

No comments:

Post a Comment