Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, January 2, 2016

KANISA LA TAG MELINZE NJOMBE LAWATAKA WAUMINI KUFANYA KAZI KWA BIDII MWAKA 2016 KUINUA UCHUMI WAO



MCHUNGAJI WA KANISA LA TAG MELINZE  TWEVE AKIWA KANISANI KWAKE  AKIHUBIRI NENO LA UZIMA

 

 MCHUNGAJI WA  KANISA LA TAG ITUNDUMA KATA YA MTWANGO  WILAYA YA NJOMBE ZAKAYO MBOKA AKITOA INJILI KATIKA KANISA LA TAG MELINZE
 
 WAUMINI WA KANISA LA TAG  WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA NENO LA YZIMA KANISANI HAPO


 MCHUNGAJI ZAKAYO MBOKA ANAHUBIRI NENO

 WAUIMBAJI WA KWAYA YA  KUTOKA MTWANGO




 MUIMBAJI BINAFSI






SAMWELI TWEVE KIJANA HUYO ANAYEONEKANA AMETANUA MIGUU KWA FRAHA AKICHEZA  PAMOJA NA WAIMBAJI WENGINE WAKIWA KANISANI HAPO
 MUIMBAJI BINAFSI HENRY DANFORD  MHEMA  AKIWAPAGAWISHA WAUMINI NA NYIMBO ZAKE ZILIZOPO KWENYE ALBAM YAKE YA MAPITO










 WACHUNGAJI HAO WANAWAOMBEA WENYE SHIDA MBALIMBALI KANISANI HAPO




MAPEPO WANAONDOLEWA KWA WENYE SHIDA MBALIMBALI



Waumini Wa Kanisa La TAG Wilaya Ya Njombe Wametakiwa Kwenda Kuuanza Mwaka Mpya  Kwa Kuongeza Jitihada Mbalimbali Za  Kilimo Cha Kibiashara Na Kushiriki Shughuri Za Ufugaji Wa Kuku Na Mifugo Mingine Ili Kukuza Uchumi Wao Na Kuleta Manufaa Kwa Waumini Wa Kanisa Hilo.

Kauli Hiyo  Imetolewa Na Mchungaji Wa Kanisa La Tanzania Assembles Of God  Lililopo Mtaa Wa Melinze Cefania Tweve Wakati Akizungumza Na Uplands Fm Mara Baada Ya Ibada Ya Jumapili Iliyofanyika Kanisani Hapo Na Kusema Kuwa  Kanisa Linafrahi Kuona Waumini Wanakuwa Na Uchumi  Mzuri  Na Kufanikisha Kuwasomesha Watoto Wao.

Aidha Mchungaji Tweve Amesema  Ujasiliamali Unawasaidia Wakristo   Kulitangaza Jina La Mungu   Tofauti Na Wakiwa Hawana Shughuli Za Kuinua Uchumi Wao  Wengine Wanaweza Kujihusisha Na Swala La Ulevi ,Ujambazi Na Wengine Kushindwa Kuwasomesha Watoto Wao   Jambo Ambalo Biblia Inakataza Tabia Hizo.

Kwa Upande Wake Mchungaji Wa Kutoka Kanisa La TAG  Itunduma Kijiji Cha Wangama Kata Ya Mtwango Zakayo  Ngoga Amesisitiza Wakristo Kudumisha Matendo Mema Kwa  Jamii Mbalimbali Ambako Wanaishi Ili Wawe Barua  Na Mwanga Kwa Watanzania Katika Kulihubiri Neno La Kristo Huku Akikemea Tabia Za Ukahaba Kuwa Siyo Mapenzi Ya Mungu.

Mchungaji Ngoga Amesema Kumaliza Mwaka  Isiwe Fursa Kwa Wakrito Kuruhusu Maovu Kufanyika Katika Jamii  Badala Yake Wakemee Tabia Ovu Katika Maeneo Wanayoishi  Kwa Kutoa Taarifa Za Uharifu Sehemu Husika  Ili Kuishi Kwa Amani Na Utulivu  Nakwamba  Kipindi Hiki Maadili Kwa  Vijana Yameshuka  Ambapo Inapaswa Kukemewa Na Watumishi Wa Dini Na Serikali.

No comments:

Post a Comment