HAWA NI WASHIRIKI WA SEMINA HIYO ILIYOSHIRIKISHA MIKOA MITATU LAKINI MMOJA HAUJAHUDHURIA MKOA WA RUVUMA
KATIBU MTENDAJI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA USHIRIKA TANZANIA WILGIS MBOGORO AKITOA SEMINA YA SIKU MOJA ILIYOFANYIKIA NJOMBE MJINI
WASHIRIKI WA SEMINA HIYO
AFISA USHIRIKA NA MRAJIS WA VYAMA VYA USHIRIKA MKOA A NJOMBE EXAUD SAPALI AKITROA NASAHA ZA USHIRIKA AKIWA NDIYE MWENYEJI KATI YA WASHIRIKI WOTE.
MWENYEKITI WA NJORUMA MKOA WA NJOMBE CREMENCE MALEKELA AKIZUNGUMZA NAYE NA WASHIRIKI WA SEMINA HIYO.
AFISA USHIRIKA MANISPAA YA IRINGA BI.ASSA CHUMA MKOCHA
THEOFRID TOLAGA KATIBU WA USHIRIKA WA UPANGISHAJI NYUMBA MANISPAA YA IRINGA AKIZUNGUMZA MBELE YA WANASEMINA HAO
AFISA USHIRIKA WA HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE
KATIBU MTENDAJI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA USHIRIKA TANZANIA WILLIGIS O.MBOGORO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA SEMINA KUMALIZIKA
Shirikisho La Vyama Vya Ushirika Nchini Leo Limehitimisha Semina Ya Ufuatiliaji Juu Ya Ununuzi Wa Hisa Za Jengo La Ushirika Lililopo Mtaa Wa Mnazi Mmoja Jijini Dar Es Salaam Ambayo Imevikutanisha Vyama Hivyo Kutoka Mikoa Ya Iringa, Njombe Na Ruvuma Ambayo Imehitimishwa Mjini Njombe.
Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Mara Baada Ya Kuhitimisha Semina Kwa Vyama Vya Ushirika Vya Mikoa Hiyo Ya Iringa Njombe Na Luvuma Katibu Mtendaji Wa Shirikisho La Vyama Vya Ushirika Tanzania Willigis O. Mbogoro Amesema Chimbuko La Uwekezaji Wa Pamoja Ulianzia Mkoa Wa Dodoma Baada Ya Mkutano Wa Ushirika Nchi Nzima Kuweka Azimio La Uwekezaji Wa Pamoja Wa Ushirika.
Aidha Bwana Mbogoro Amesema Lengo La Kuanzisha Dhana Ya Uwekezaji Wa Pamoja Ni Kutaka Vyama Vyote Vya Ushirika Na Wanachama Wa Vyama Hivyo Waweze Kunufaika Baada Ya Kugundua Kuwa Mfumo Uliopo Hauwanufaishi Wanachama Na Vyama Vyao Vya Ushirika Kutokana Na Kutegemea Uwezo Wa Kimtaji Kutoka Kwenye Taasisi Za Kifedha Na Makampuni Mengine Katika Kutoa Huduma Za Shirika.
Amesema Wameanzisha Dhana Hiyo Ya Uwekezaji Wa Pamoja Kwa Kuanzia Na Jengo Hilo La Ushirika Ambalo Semina Na Mikutano Yake Ya Kuelimisha Wanachama Tangu Mwezi Mei Mwaka Huu Ili Jengo Hilo Liweze Kumilikiwa Na Wanaushirika Wenyewe Ambapo Tarehe 31 Mwezi Decemba Wanahitimisha Zoezi La Ununuzi Wa Hisa Kwa Kila Mwanachama.
Baadhi Ya Washiriki Wa Semina Hiyo Wameshindwa Kufikia Malengo Ya Kuhamasisha Wanachama Kununua Hisa Kwa Wingi Na Kufikia Kiasi Cha Fedha Zisizopungua Milioni Tano Kwa Kila Chama Kutokana Na Jiografia Ya Maeneo, Fomu Kuandikwa Kwa Lugha Ya Kingereza Na Kiwango Kikubwa Cha Kununulia Hisa Huku Mkoa Wa Iringa Ukifanya Vizuri Katika Ununuaji Huo.
No comments:
Post a Comment