MADUKA YA NJOMBE MJINI YAKIWA YAMEFUNGWA HADI MUDA HUU
NI KESI YA MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA JWT JONSON MINJA IMESABABISHA MADUKA KUFUNGWA
HALI ILIVYO HIVI NJOMBE
HAPA NI ENEO LA KITUO KIKUU CHA MABASI NJOMBE NAPO WAMEFUNGA BAADHI YA WAFANYABIASHARA
Wakati
Taifa la Tanzania Likitarajiwa Kushuhudia Adha Kubwa ya Kufungwa Kwa
Maduka Kwa Takribani Nchi Nzima Kwa Muda wa Siku Tatu Kuanzia Leo ,Wananchi Mkoani Njombe Wamewaomba Wafanyabiashara Hao Kuangalia
Namna ya Kufungua Maduka Hayo Wakati Kesi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wafanyabiashara Taifa Ikisikilizwa Mjini Dodoma.
Kesi
ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya JWT Bwana Johnson Minja Ilipangwa
Kusikilizwa Kwa Muda wa Siku Tatu Mfululizo Katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi Dodoma Siku Ambazo Wafanyabiashara Watakwenda Kufunga Maduka Yao.
Kituo
Hiki Kimezungumza na Baadhi ya Wananchi Mjini Njombe Juu ya Adha
Itakayojitokeza Endapo Maduka Hayo Yatafungwa Kwa Siku Zote Kuanzia
Juni Nane Hadi Kumi Mwaka Huu Huku.
Wengine
Wamesema Kuwa ni Vyema Serikali Ikiangalia Namna ya Kutatua Tatizo
Hilo Haraka Iwezekanavyo Badala ya Kuendelea Kushuhudia Maduka
Yakifungwa Kutokana na Tatizo la Mashine za EFD.
Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Taifa Johnson Minja Akizungumza na Kituo Hiki Kwa Njia ya
Simu Toka Mkoani Dodoma Amesema Kuwa Utaratibu Rasmi Utafahamika Kesho
Baada ya Mahakama Kuzungumza Chochote Kama ni Kweli Kesi Hiyo Itakwenda
Kwa Siku Zote Tatu Au Itaahirishwa.
Minja
Amesema Kuwa Licha ya Kuwepo Kwa Maombi ya Wananchi na Wateja Wao Juu
ya Kutofunga Maduka Hayo Lakini Hata Yeye Amekuwa Akiwataka
Wafanyabiashara Hao Kufungua Maduka Bila Mafanikio Mbali na Kwamba Hata
Wao Wanapata Hasara Kubwa.
No comments:
Post a Comment