Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, June 7, 2015

WAZAZI WATAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI MEMA,MIAKA MITANO MTOTO KUSOMA BWENINI HADI CHUO KIKUU MAADILI YA NAHARIBIKA


 MTOTO JACKRINE MGAYA AKITOA SOMO LA INJILI KATIKA KANISA LA T.A.G
 WALIMU WA WATOTO AKIWEMO HENRY NDONE AKIWA NA MWENZAKE  NJE YA KANISA WAKIJADILI BAADA YA IBADA KUMALIZIKA







 WATOTO WAKIWA KANISANI PAMOJA NA WAUMINI WENGINE




 MAMA MCHUNGAJI TWEVE  AKITOA MAELEKEZO KIDOGO

 MTOTO JACKRINE MGAYA AKISOMA INJILI  MBELE YA MCHUNGAJI TWEVE














 waumini hapa wanatoka Baada Ya Ibada Kumalizika

Wazazi Na Walezi Wametakiwa Kutoa Huduma Za Msingi Kwa Watoto Iikiwemo Elimu,Malazi, Huduma Za Kiroho  Na Ulinzi  Pamoja Na Kuacha Tabia Ya Unyanyasaji Na Ukatili Kwa Watoto Wao   Ili Kujenga Taifa Lenye Maadili Ya Kikristo Nchini .

Rai Hiyo Imetolewa Na Mchungaji Wa Kanisa La Tanzania Asembles Of God TAG Lililopo Mtaa Wa Menze Cefania Tweve Wakati Akiongea  Na Waumini  Wa Kanisa Hilo  Katika Ibada Ya Kwanza  IKiwa Ni Sikukuu Ya Watoto  Nchini Katika Kanisa Hilo Nchini.

Aidha Mchungaji Tweve Amesema Kuwa  Wazazi Wanatakiwa Kuepuka Tabia Ya Kupeleka Watoto Kwenda Kuishi Na Ndugu Zao  Na Kuwatumikisha Kazi Za Ndani  Ambapo Amesema Kuna Baadhi Ya Wazazi Wamekuwa Wakiwatesa Kwa Kuwanyima  Chakula  Huku Akishaauri  Wazazi Kuwaelimisha Na KuWazoesha Katika Shughuli Za Kilimo Kwa Manufaa Yao Ya Baadaye.

Mchungaji Tweve Ametaka Wazazi Kuakagua Wanako Lala Watoto Wao Na Kuweka Mazingira Mazuri Huku Akikemea  Vikali Tabia Ya Baadhi Ya Wazazi Kuwapeleka Watoto Wadogo Kuanzia Miaka Mitano Kuishi Bwenini Hadi Chuo Kikuu  Kwa Madai Wanakosa Malezi Ya Mama Na Baba Na Kufanya Kuiga Utamaduni Wa Kigeni Ikiwemo Kuvaa Mavazi Yasiostahili.

Katika Neno La Injili Kanisani Hapo Kwa Niaba Ya Watoto Wengine Jackrine Mgaya  Amesema Watoto Wanatakiwa Kuwaheshimu Wazazi Ili Waishi Miaka Mingi Na Hri Duniani,Kuwa Na Tabia Njema Kwa Wakubwa Huku Wazazi Nao Wakitakiwa Kuwajali Watoto Na Kuwapatia Heshima Zao Zote.

Akisoma Risala Kwa Niaba Ya Watoto Wote Akiwa Kanisani hapo  Musa Chami Amesema Kuwa Watoto  Wanaomba Kutengewa  Darasa Lao Kuliko Kuchanganyikana Na Wakubwa,Walimu Wao Kutiwa Moyo Hata Kwa Maneno Ya Faraja Kwani Wanawafundisha Vizuri,Viti Vya Kukalia Watoto Havipo,Watoto Wakifundishwa Vizuri Biblia Ndilo Kanisa La Baadaye Huku Wakichangia Shilingi Laki Tano Kwaajili Ya Kumtia Moyo Mchungaji Na Kanisa Zima La T.A.G Melinze.

No comments:

Post a Comment