Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, February 6, 2015

WATU WANNE WANAOSADIKIKA KUWA NI MAJAMBAZI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE

 
 KAMANDA NGONYANI AKIWA OFISINI KWAKE

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Linawashikilia   Watu Wanne Kwa Tuhuma Za  Unyang'anyi Wa Mali Kwa  Kutumia Nguvu  Katika Tukio Ambalo Limetokea Jana Njiapanda Ya Magereza  Baada Ya Kumvamia Na Kumpora Fedha Shilingi Milioni Tano Mfanyabiashara Cecelia Mwalongo Na Kukimbia Na Gari Lao Kuelekea Luvuma.

Kamanda Wa Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe SACP Fulugence Ngonyani Amewataja Watuhumiwa  Hao Kuwa Ni Pamona Na Jumanne  Makumbati Mwenye Umri Wa Miaka 40,Joram Gerelota Mwenye  Umri Wa Miaka 44,Alfred  Stima Warioba Mwenye Umri Wa Miaka 28 Na Chagari Mwenda Wote Wakazi Wa Jijini Dar Es  Salaam.

Aidha Kamanda Ngonyani Amesema Kuwa  Watuhumiwa Hao Walifanya Tukio Hilo  Mnamo Februari 2 Majira Ya Saa Sita Na Nusu   Wakiwa Na Gari  Aina Ya Toyota Lenye  Namba Za Usajiri T410 CFQ Rangi  Ya Silva  Aina Ya Toyota  IST  Ambalo Limehifadhiwa Kituoni Ambapo Baada Ya Kumvamia Na Kupora  Fedha Hizo Na Kisha Kukimbia Kuelekea Barabara Ya Njombe Luvuma.

Amesema Kuwa  Watuhumiwa Hao Walikamatwa Baada Ya Ushirikiano Mkubwa Na Wananchi Wa Njombe  Na Jeshi La Polisi Hadi Walipofanikiwa Kuwakamata Mpakani Mwa Mkoa Wa Njombe Na Luvuma Ambako Wananchi Waliwasiliana Na Wananchi Wa Luvuma Na Kuweka Vizuizi Barabarani Na Kufanikiwa Kuwakamata.

No comments:

Post a Comment