Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, February 6, 2015

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA UTOAJI HAKI MKOANI NJOMBE

 

 KAIMU MKUU WA MKOA WA NJOMBE AMBAYE NI MKUU WA WILAYA YA NJOMBE BI.SARAH DUMBA AKITOA HOTUBA YAKE

Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Amesema Serikali Inaendelea Na Jitihada  Za Kuboresha   Maeneo Ya  Utoaji Haki Ikiwemo Madawati Ya Jinsia Na Hatua Mbalimbali Za Kufikia Mahakama Katika Mashauri  Ya Jinai,  Rushwa  Ambapo Wadau Wa Sheria Nao Wanapaswa Kutii  Na Kuheshimu Sheria Za Nchi.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Bi.Sarah Dumba   Kwa Niaba Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Wakati Wa Siku Ya Sheria Nchini   Ambayo Kwa Mkoa Wa Njombe Imefanyika Katika Mahakama Ya Wilaya Ya Njombe  Na Kusema Kuwa Haki Inakwenda Na Wajibu Na Wadau Watimize Wajibu Wao Kwa Manufaa Ya Jamii Nzima.

Bi. Dumba Amesema Ujumbe Wa Mwaka Huu Umeelekeza Kwa Wananchi Kutii Sheria Za Nchi,Kuepuka Kutengeneza Jinai Na Uharifu Kwa Lengo La Kudumisha Amani Na Utulivu,Kukabiliana Na Athali Zinazotokana Na Utandawazi Na Mmomonyoka Wa Maadili  Kwa Maslahi Ya Kudumisha Mila,Tamaduni Na Desturi Nzuri Zinazojenga Uzarendo Na Umoja Wa Taifa.

Amesema Kuwa  Serikali Imekuwa Ikiendelea Na Jitihada Za  Kutoa Fursa Ya Uhuru Wa Mahakama Kwa Kuhakikisha  Maeneo Yake Yanaboreshwa  Ambapo  Uboreshaji Wake Utakwenda  Awamu  Kwa Awamu  Kuboresha Mazingira Yake .

Kwa Upande Wake Hakimu Mkazi Mfawidhi Wa Mahakama Ya Wilaya  Ya Njombe Augustino Rwezile Amesema Kuwa Mahakama Hiyo  Hapo Mwakajana Kulikuwa Na  Mashauri  YA Muda Mrefu  Sabini Na Tano   Ambapo Mwaka Huu Wanamashauri Matatu Ambayo Ni Ya Mwaka 2013.

Hakimu Rwezile Amepongeza Jeshi La Polisi Kwa Jitihada Kubwa Zilizofanyika Katika Kipindi  Cha Mwaka 2014 Za Kuhakikisha  Uchunguzi Wa Mashauri   Mbalimbali   Unakamilika  Ambapo Hali Hiyo Inasaidia Kuondoa Dhana Ya Wananchi  Kusema Kesi Ikienda Mahakamani  Lazima Rushwa Itolewe Ndipo Haki Itendeke.


Kauli Mbiu Ya Mwaka Huu Inasema "Fursa Ya Kupata Haki,Mchango Na Wajibu Wa Serikali,Mahakama Na Wadau" Ambapo  Kutokana Na Mada Hiyo  Inatoa Wasaa Wa Kujadili  Mambo Makuu  Mawili Ambayo Ni  Fursa Ya Kupata Haki, Mchango Na Wajibu Wa Serikali,Mahakama Na Wadau.

No comments:

Post a Comment