Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, December 1, 2016

SHIRIKA LA HIGHLANDS HOPE UMBRELLA LA TUA ITULIKE NJOMBE

 
 MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA ITULIKE BWANA NG'ANDE AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MTAA WAKE


 WANANCHI WA MTAA WA ITULIKE WAKISIKILIZA KWA UMAKINI


MUKUFUNZI WA SHIRIKA LA HIGHLANDS HOPE UMBRELLA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI KUHUSIANA NA KERO ZINAZOIKABILI SEKTA YA AFYA KWA AKINA MAMA NA WATOTO KWENYE ZAHANATI NA VITUO VYA AFYA NA HOSPITALI
NJOMBE

Muuguzi wa  zahanati ya Itulike Monica Mwakipesile amewataka wananchi wa mtaa huo kujiunga kwenye mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya CHF Kwaajili ya Kupatiwa matibabu kwa mwaka mzima unaoshirikisha watu sita katika familia moja.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa mtaa huo B.Mwakipesile amesema ili zahanati iweze kuwa na dawa za kutosha katika zahanati wananchi wanatakiwa kuchangia mfuko huo ambapo pesa hizo zitatumika kununulia dawa za kuwapatia wagonjwa  wanaokwenda  kutibiwa.

Bi.Mwakipesile amesema tatizo la kukosekana kwa dawa lililokuwepo hapo awali litakwenda kumalizika  ambapo amesema ni watu 28  wa mtaa wa Itulike waliotekeleza zoezi la uchangiaji mfuko huo ikiwa mtaa unawatu wengi .

Kuhusu Huduma za matibabu bure kwa wazee Bi.Mwakipesile amesema zahanati hiyo haiwezi kuwapokea wazee wa aina yoyote ile watakaokwenda kupatiwa huduma za matibabu endapo watakuwa hawana vitamburisho vya kupatiwa matibabu bure  ya wazee hao.

Baadhi ya wazee wa mtaa wa Itulike wamesema wapo tayari kutofika kwenye zahanati hiyo hata kama wamezidiwa kutokana na serikali kushindwa kutoa vitamburisho vya matibabu bure huku wananchi wakiwa na hofu juu ya kutoa shilingi elfu kumi kwaajili ya Bima ya afya kwa kile walichodai kukosa dawa kwenye zahanati hiyo.


Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Itulike Michael Ng'ande amewahakikishia wazee hao kwamba serikali itaendelea kufuatilia vitamburisho hivyo kutoka kwa viongozi wa halmashauri ili wapate huduma za matibabu kwenye zahanati hiyo.

Mkutano huo ambao umesimamiwa na shirika la Highlands Hope  Umbrela unatarajia kuendelea katika mitaa mbalimbali ya kata za mjini Njombe lengo likiwa kupata changamoto ya afya inayowakabili akina mama na watoto.

No comments:

Post a Comment