Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, December 10, 2016

DC NJOMBE ATAKA HALMASHAURI YA MJI KUWAGAWIA VIJANA VIWANJA VYA KUJENGA NYUMBA ZAO

                     
 MKUU WA WILAYA YA NJOMBE BI.LUTH ,MSAFIRI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI .

NJOMBE

Halmashauri ya mji wa Njombe Imetakiwa kuacha kugawa viwanja kwa upendeleo na kulifikilia kundi la vijana katika kusaidia kuwapatia viwanja  hivyo kwaajili ya kujenga nyumba zao   kuliko kugawa kwa wachache kama ilivyo kwa sasa.

Hayo yamesemwa na Vijana mjini Njombe  mbele ya mkutano wa mkuu wa Wilaya  ambapo wamepeleka malalamiko yao ya kushindwa kupewa viwanja na Halmashauri hiyo ambavyo vimepimwa vinauzwa kwa bei kubwa  kuanzia shilingi milioni nne hadi milioni 14 bei ambayo vijana  na wananchi wanashindwa kumudu gharama zake.

Diwani wa kata ya Njombe Mjini Agrey Mtambo amesema sababu inayofanya vijana na wananchi wengine kushindwa kununua viwanja hivyo ni gharama kuwa kubwa na kuiomba halmashauri ijaribu kupunguza bei ya Viwanja ili Vijana na wananchi wengine  wenye uwezo wa chini wanufaike navyo.

Akijibu maswali ya vijana hao kuhusiana na Viwanja hivyo afisa ardhi wa halmashauri ya mji wa Njombe Thadei  Kabonge amesema viwanja hivyo havikugawiwa kwa upendeleo wowote  bali viliuzwa kwa kila mmoja  mwenye uwezo wa kuvinunua  Huku mkurugenzi akisema mwaka 2012  viwanja vilipimwa ambapo bado hadi sasa vingine havijapata watumiaji .

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Luth Msafiri ameagiza halmashauri hiyo kutoa viwanja vyote kwa wananchi na kuwatangazia wananchi kwamba viwanja vimekwisha na vimeuzwa kwa utaratibu wa serikali  ambapo ameshindwa kuridhika na majibu ya Afisa ardhi wa Mji kwamba tangu wapime mwaka 2012 ikiwa ongezeko la watu lipo kila mwaka.

No comments:

Post a Comment