Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, December 22, 2016

CHADEMA TAIFA WAKAGUA MIRADI YA VYOO NA VIBANDA VYA BIASHARA RAMADHANI NJOMBE MJINI


 
 KATIBU MKUU CHADEMA TAIFA VINCENT MASHINJI AKISALIMIANA NA BIBI MAGDALENA WA RAMADHANI NJOMBE ALIPOTEMBELEA KUKAGUA MIRADI YA VYOO NA VIBANDA VYA BIASHARA VINAVYOJENGWA KWENYE MTAA HUO VIKIWA CHINI YA MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA BATHROMEO KYANDO ALIYECHAGULIWA KUPITIA  TIKETI YA CHADEMA.
 HAPA KATIBU MKUU AKIZUNGUMZA NA MBUNGE WA VITI MAALUMU MKOA WA NJOMBE {CHADEMA} LUCIA MLOWE WAKIWA  KWENYE MRADI WA VIBANDA VYA BIASHARA UNAOTEKELEZWA MTAA WA RAMADHANI.

 KATIBU MKUU WA CHADEMA TAIFA VINCENT MASHINJI AKIZUNGUMZA NA MWENYEKITI WA MTAA WA RAMADHANI  BATHROMEO KYANDO ALIYESHIKANA MIKONO

 HIVI NI VYOO AMBAVYO VIMEJENGWA CHINI YA USIMAMIZI WA MWENYEKITI HUYO ALIYETEMBELEWA NA VIONGOZI CHADEMA TAIFA.
 HIVI VYOO NDIVYO VILIVYOKUWA VIKITUMIKA KABLA YA VIPYA KUKAMILIKA

 MBUNGE WA IRINGA MJINI CHUNGAJI PETER MSIGWA AKIZUNGUMZA NA WAKAZI WA RAMADHANI NJOMBE MJINI
 VIBANDA HIVYO VYA SERIKALI YA MTAA WA RAMADHANI AMBAVYO NI MRADI WA SERIKALI  NA KATIKATI NI JENGO LA OFISI YA MTAA NALO LINANDELEA KUJENGWA LAKINI LIMEPAULIWA.



 SHANGWE NA NDEREMO ZA AKINAMAMA WAKISHANGILIA KWA FRAHA BAADA YA KUTEMBELEWA NA VIONGOZI CHADEMA TAIFA.

 HAPA NI ENEO LA KIWANJA CHA OFISI YA CHADEMA MKOA INAPOTARAJIA KUJENGWA
 KATIBU CHADEMA MKOA WA NJOMBE ALATANGA NYAGAWA AKIZUNGUMZA KABLA YA KUMKARIBISHA KATIBU MKUU CHADEMA TAIFA.
 MBUNGE  VITI MAARUMU MKOA WA NJOMBE  LUCIA MLOWE AKIMSIKILIZA KATIBU KWA UMAKINI.



 KULIA NI DIWANI WA KATA YA RAMADHANI NA KUSHOTO NI MBUNGE VITI MAALUMU MKOA LUCIA MLOWE WALIWA ENEO LA KIWANJA CHA OFISI YA CHADEMA MKOA WA NJOMBE LUNYANYWI.



 MWENYEKITI WA BARAZA LA WAZEE TAIFA  HASHIMU JUMA ISSA AKIZUNGUMZA NA WANANJOMBE.




 AKINA MAMA WA NJOMBE WAKIWA NA FRAHA KUBWA

 HILI NI ENEO LA UKUMBI WA MLIMANI MOTEL









 MADIWANI WAKISIKILIZA KWA UMAKINI AKIWEMO DIWANI WA KATA YA RAMADHANI GEOGE MENSON SANGA  KULIA



 KATIBU MKUU CHADEMA TAIFA VINCENT MASHINJI AKIZUNGUMZA NA WANA NJOMBE KATIKA UKUMBI WA MLIMANI MOTEL


 MWANASHERIA  WA KUJITEGEMEA ENOS SWALE AKIZUNGUMZA KWA NIABA YA WANA LUPEMBE





NJOMBE

Katibu Mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Taifa Dr. Vincent Mashinji  ametembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya vyoo na vibanda vya biashara vilivyopo Mtama wa Ramadhani Mjini Njombe.

Dr. Mashinji amepongeza Serikali ya mtaa  wa Ramadhani akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya Mtama huo Bathromeo Kyando na Diwani wake George menson Sanga waliochaguliwa kupitia CHADEMA kwa kutekeleza miradi Mkubwa ukiwemo wa vyoo ulioghalimu zaidi ya shilingi milioni 30 na vibanda vya Serikali ya Mtama ambavyo vinaendelea kujengwa.

Mradi huo unaosimamiwa na Diwani na Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa iliyopo chini ya CHADEMA umefiki hatua za nzuri na utakamilika muda wowote kuanzia sasa.

Dkt Mashinji amewataka  viongozi wengine kuiga mfano wa  Serikali ya Mtama wa Ramadhani kutekeleza miradi hiyo ili mwaka 2020 waweze kuwa na nafasi ya kupata ushindi kuanzia kwenye ngazi za mitaa hadi taifa.

Aidha Dr. Mashinji amemtaka Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Njombe Lucia Mlowe wa CHADEMA kushikamana na viongozi wa kata na vijiji ili kuboresha miundombinu iliyopo huku na kumpongeza  kwa jitihada alizozianza za kununua kiwanja eneo la Hagafiro na kuanza ujenzi wake.

Kuhusu Wazee Dr. Mashinji amesema Serikali inatakiwa kuwaboreshea huduma za matibabu bure na kuongeza madawa kwenye mahospitali ili watu wote wapate huduma za matibabu kwa uhakika huku swala la elimu bure lililotangazwa na Serikali likibaki kuwa tatizo kwa kushindwa kutekeleka kama Ahadi iliyotolewa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Taifa Hashimu Juma Issa amesema CHADEMA Mkoa wa Njombe ni mfano wa kuigwa kwa kuwa na muamko wa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kutoka CHADEMA Njombe zijenge ofisi zao na kuondokana ofisi za kupanga kwa kujenga za kwao kama ilivyoanza kujenga ofisi ya chadema mkoa.

Nae Katibu CHADEMA Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa akiwa na Mwenyekiti wake Fakii Lulandala wamesema Mkoa wa Njombe umejipatia ushindi kwa kata za Mjini zote ambazo zimeonekana kufanya vizuri kuliko waliokuwepo madiwani waliopita wa CCM ambapo wanajiandaa kikamilifu kuhakikisha wanashinda kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 kwa kushinda majimbo na mitaa na kata za Njombe na Wilaya zake.

No comments:

Post a Comment