Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, November 30, 2016

MKUU WA WILAYA YA NJOMBE AKAGUA MIRADI YA HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE

 MILANGO YA VYOO VYENYE MATUNDU 8 KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA ANNE MAKINDA ILIYOPO KATA YA IHANGA






 MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI AKIONJA CHAKULA CHA WANAFUNZI WA ANNE MAKINDA ALIPOTEMBELEA
 KULIA NI MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI KATIKATI NI MKUU WA SHULE YA SEKONDARI YA ANNE MAKINDA VERONICA MLOZI NA WA KUSHOTI NI AFISA ELIMU SHULE ZA MSINGI KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE ZEGELI SHENGERO
 HUYU NI MWALIMU MKUU WA SHULE YA MSINGI MUUNGANO ILIYOPO KIFANYA  MWALIMU BABTIST SARUFU AKIZUNGUMZA NA MKUU WA WILAYA AKIWA OFISINI KWAKE
 HII NI NYUMBA YA MWALIMU NA HAWA NI WANAFUNZI WANAJIUNZA KILIMO SHULENI
 NYUMBA MPYA YA MWALIMU IMEGHALIMU MILIONI TATU  NA NGUVU ZA WANANCHI WA KIFANYA


 HII NI ZAHANATI YA KIFANYA AMBAYO MKURUGENZI AMESEMA KWA KUWA VITANDA HAVITUMIKI ATAKWENDA KUHAMISHA NA KUPELEKA SEHEMU ZENYE UHITAJI WA VITANDA




PICHA YA PAMOJA NA MKUU WA WILAYA  MKURUGENZI,MAAFISA ELIMU HASSAN IGWE,ZEGELI SHENGERO NA KATIBU TAWALA NA ASKALI WA POLISI

NJOMBE

Halmashauri ya Mji wa Njombe imetakiwa kusimamia vizuri pesa zinazopelekwa kwaajili ya  elimu bure kwa kukarabati madarasa   yaliochimbika sakafu  ili  yawe na viwango  vinavyokubalika pamoja na  nyumba za walimu zinazoendelea kujengwa .

Bi.Msafiri ametoa agizo  la kukarabati vyumba chakavu vya  madarasa  kupitia pesa za elimu bure zinazotolewa na serikali na kuwahamishia  chumba chenye hewa ya kutosha wanafunzi wa darasa la awali peluhanda  ambapo akiwa shule ya msingi Muungano ya Kifanya ameagiza kuondolewa milango iliyopo chini ya kiwango kwaajili ya nyumba  ya mwalimu.

Akiwa katika shule ya sekondari ya wasichana ya Anne Makinda Bi.Msafiri amekagua miradi ya nyumba za walimu na choo chenye matundu 8 kilichogharimu shilingi milioni 16 huku nyumba ya walimu  ikitarajia kughalimu shilingi milioni 150 hadi kukamilika kwake na kufanya jumla ya shilingi milioni 166.

Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Njombe Bi.Iluminata  Mwenda amesema darasa la awali lipo kujengwa  ambapo ameomba wananchi kuanza kusogeza tofari elfu hamsini ili Halmashauri iwaunge mkono kwa kupeleka milioni 22 Kwaajili ya darasa hilo ambapo akiwa zahanati ya kifanya ameahidi  kuondoa  vitanda visivyotumika   na kupeleka kungine.

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Luth Msafiri ametembelea shule ya msingi Mpeto  iliyopo kata ya Ramadhani,Shule ya msingi peluhanda iliyopo kata ya Mjimwema,Kituo cha kukusanyia matunda kilichopo Nundu kata ya Yakobi,Shule ya wasichana ya Anne Makinda iliyopo kata ya Ihanga na Zahanati ya Kifanya na shule ya msingi Muungano ya Kifanya.




No comments:

Post a Comment