Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, October 8, 2016

WANANCHI WILAYANI NJOMBE WAHIMIZWA KUJIUNGA NA CHF KWA MATIBABU MWAKA MZIMA

 WANANCHI WA KIJIJI CHA HAVANGA KWA UMAKINI WANASIKILIZA HOTUBA YA MBUNGE WAO  ALIPOTEMBELEA NA KUFANYA MKUTANO KIJIJINI HAPO

 AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA HAVANGA  LIVIN JOHN AKISOMA TAARIFA FUPI MBELE YA MBUNGE HUYO

 MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI YA CCM WILAYA YA NJOMBE BI.VELONICA AKIZUNGUMZA NA KUWASHUKURU WANANCHI KWA KUKICHAGUA CHAMA HICHO KUANZIA NGAZI YA WENYEVITI WA VIJIJI HADI RAIS KWENYE JIMBO HILO


 MBUNGE AKITOA HOTUBA YAKE KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA HAVANGA
 MBUNGE AMESHIKA MPIRA WA KUWAPATIA VIJANA WAENDELEZE MICHEZO

 VIFAA VYA MICHEZO MBUNGE HONGORI AKIKABIDHI KWA VIJANA WA KIUME NA WA KIKE
 KIONGOZI WA TIMU YA MPIRA WA MIKONO KUTOKA KIJIJI CHA HAVANGA AKITOKA BAADA YA KUPOKEA MPIRA NA MBUNGE IULI WANAWAKE NAO WASHIRIKI MICHEZO

 WANANCHI WALIOFIKA KWENYE MKUTANO HUO WAKISIKILIZA KWA UMAKINI

 MWENYEKITI WA SERIKALI YA KIJIJI CHA HAVANGA BWANA PHILIMON DAUD MUMUSI AKIFUNGUA MKUTANO
 MBUNGE WA JIMBO LA LUPEMBE JORAM HONGORI AKIONGEA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA HAVANGA KUHIMIZA WAJIUNGE NA MFUKO WA CHF






NJOMBE

Wananchi Wilayani Njombe wametakiwa kujiunga na  mfuko wa taifa wa afya CHF Kwaajili ya kupata huduma za matibabu  kwa kuchangia shilingi elfu kumi kwa mwaka ili kunufaika na  matibabu bure kupitia mfuko huo.

Kauli hiyo imetolewa na Mbunge wa jimbo la Lupembe Joram Hongori wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea vijiji na kata za jimbo hilo kukagua miradi na kushukuru wananchi kwa kumchagua na kusema kuna umihimu mkubwa kwa wananchi kujiunga na mfuko huo kwa kuchangia shilingi elfu kumi kwa mwaka.
 
Mwalimu Hongori amesema viongozi wa serikai za vijiji wanatakiwa kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo huku akisema swala la kukosekana kwa dawa kwenye vituo vya afya,zahanati na hospitali serikali ina mpango wa kuanzisha maduka maalumu karibu na hospitali ili kuhakikisha kila mwananchi ananunu dawa kwa bei ya ruzuku pindi dawa zinapokuwa zimekosekana hospitralini.

 Awali akisoma taarifa fupi mbele ya Mbunge huyo afisa mtendaji wa kijiji cha Havanga kata ya kidegembye Livin John amesema wananchi wa kijiji hicho wanakabiliwa na changamoto ya ujenzi wa zahanati ambayo walikwisha kuanza ujenzi wake.

Kwa upande wao wananchi wa kijiji cha Havanga wamelalamikia kuvunjwa kwa jengo la zahanati walilokwisha kamilisha ujenzi wake kutokana na uzembe wa mhandisi wa Wilaya hiyo kushindwa kwenda kukagua maendeleo yake na kusababisha kujengwa tofauti na viwango vya halmashauri ikiwa ramani alipeleka mwenyewe.

 Katika kuunga mkono jitihada za wananchi wa kijiji cha havanga za kujenga zahanati hiyo mbunge wa jimbo la lupembe ameahidi kuchangia shilingi laki tatu kwaajili ya kusombea mawe ya kujengea msingi ili kusukuma maendeleo ya kijiji na kuboresha huduma za afya.


No comments:

Post a Comment