Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, October 9, 2016

WANANCHI WA HAVANGA WALIA BARABARA YA HAVANGA IDUNDA


 
 GARI LIKIWA KWENYE VUMBI  LA BARABARANI
 


 HII NI BARABARA AMBAYO WANANCHI WAMELALAMIKIA KWAMBA HAIJAMWAGIWA MAJI WALA KUSHINDILIWA NA KUSABABISHA VUMBI KUONGEZEKA
 vumbi  la kwenye  barabara  hiyo








Wananchi wa kijiji cha Havanga kata ya kidegembye wilayani Njombe  wameiomba halmashauri hiyo kurudia kutengeneza barabara ya Havanga Idunda  kwa kushindilia na kumwagia maji kuliko ilivyo kwa sasa.
Rai hiyo imetolewa na wananchi wa kijiji hicho kufuatia kukithili kwa vumbi  ambapo wametoa kilio chao kwenye mkutano wa hadhara  wa Mbunge wa jimbo la Lupembe Joram Hongori alipotembelea katika kijiji hicho kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa.

Wamesema halmashauri ya Wilaya ya Njombe Kupitia  Mhandis wake wa ujenzi wamelima barabara hiyo bila kuwagia maji na kushindilia na kusababisha madhara kwa wananchi hususani pindi magari  yakipita yanatimu vumbi  kama unavyotazama kwenye picha hizo.

Akijibu mwaswali ya wananchi hao Mbunge wa jimbo la Lupembe Joram Hongori ameahidi kufuatilia kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe Ili kuhakikisha wanarudia kuitengeneza barabara hiyo kwa kushindilia na kumwagia maji barabara hiyo kwa kiwango kinachostahili.
Hongori amesema serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni nane kwaajili ya kutengeneza barabara ya Kibena hadi madeke kwa kiwango cha lami ili kuondoa adha inayowakuta wananchi wa lupembe kwa kipindi hicho na msimu wa kusafirisha mazao na pia barabara hiyo itaunganisha na Mkoa wa Morogoro -Mlimba.


No comments:

Post a Comment