Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, October 18, 2016

WANAFUNZI SABA WAJERUHIWA KUFUATIA UPEPO MKALI KUEZUA PAA LA SHULE


Na Editha Karlo, wa blog ya jamii,Missenyi

SHULE ya msingi Byamutemba iliyopo katika kata ya Nsunga Wilayani Misenyi imefungwa kwa muda wa wiki tatu baada ya shule hiyo mapaa ya shule hiyo kuezuliwa na upepo mkali.

Tuki hilo limetokea leo majira ya mchana wakati wanafunzi wakiendekea na masomo darasani na kusababisha baadhi ya wanafunzi kujeruhi.Upepo huo umeezua mapaa ya shule hiyo nyumba moja ya mwalimu pamoja na nyimba tatu za wakazi wa kijiji cha Byamutemba.

Mganga msaidizi wa Wilaya ya Missenyi Godon amekiri kupokea wanafunzi hao waliojeruhiwa 14 na wanafunzi 7 wakirudishwa nyumbani baada ya kupatiwa matibabu kwenye Zahanati ya Igayaza.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Luteni Kanali Denis Mwila alisema kuwa wameifunga shule hiyo kwa miezi mitatu wakati wanafanya utaratibu wa kuijenga shule hiyo kwa haraka.

Alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 903.
Shule ya msingi Byamutemba iliyoko kata Nsunga Wilayani Missenyi imeezuliwa na upepo mkali na kupelekea Wanafunzi saba kujeruhiwa,kufuatia tukio hilo, shule hiyo kwa sasa imefungwa kwa muda.
Baadhi ya Wanafunzi wakiwa wamelazwa katika Zahanati ya Igayaza,baada ya kujeruhiwa na tukio hilo
Baadhi ya wananchi wakijadiliana jambo kufutia shule hiyo kuezuliwa na upepo mkali .
 

No comments:

Post a Comment