Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, October 4, 2016

ASKARI POLISI WA RUSHWA ZANZIBAR APOTEZA KAZI


indexKufuatia kitendo cha askari namba  F. 3016 SGT Talib Hamad Kassim ambaye tayari amefukuzwa kazi na Jeshi la Polisi kwa kitendo chake cha kuomba na kupokea  rushwa kutoka kwa raia wa kigeni mjini Zanzibar, Jeshi la Polisi nchini linalaani vikali tabia hiyo na kwamba ni tabia ya askari binafsi na siyo maadili ya askari wa Jeshi la Polisi.

Kutokana na kitendo hicho, tayari Jeshi la Polisi limemfukuza kazi askari huyo na atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria. Aidha, Jeshi la Polisi litaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya askari wake yeyote atakayekiuka maadili yake ya kazi.

Jeshi la Polisi nchini halitamuonea muhali askari yeyote atakayekwenda kinyume na maadili ya kazi na kutenda vitendo binafsi vinavyo lifedhehesha au kulitia dosari Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Advera John Bulimba – ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.     

No comments:

Post a Comment