Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, August 29, 2016

MJUE KIUNDANI DIKTETA MZALENDO NA MTANASHATI MUAMAR GADDAFI

Imeandikwa na Geofrey Chambua 


Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.


Baada ya kuuawa kwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, walibya na dunia kwa ujumla imeingia katika mitizamo tofauti kuhusu kiongozi huyo huku wengine wakikumbuka mafanikio aliyoleta kwa taifa na wengine wakiangalia picha ya pili ya udikteta wake; 


Unajua ni kwanini Walibya na Afrika ilimlilia Gaddafi?



Mzaliwa wa Juni 7, 1942, 'mtoto wa mfugaji, Muammar Mohammed Abu Minyar Gaddafi alijikuta Raisi wa Libya miaka

27 tu baadae kwani mnamo mwaka 1967 aliingia madarakani kwa kumpindua 'King' Iddris akiyaita mapinduzi ya kiutamaduni-Mapinduzi haya yalimpa jina la shujaa mtanashati (Handsome Hero) kwani alifanya mapinduzi bila kumwaga damu

Haya ni baadhi ya mambo ambayo Gaddafi aliyasimamia na kuyatekeleza katika utawala wake wa miaka 42 kwa Libya.



1. Chini ya Utawala wake Walibya walineemeka haswaaa kwani licha ya elimu, umeme, afya na mahitaji mengine ya msingi kuwa BURE, Kwa waliokuwa wakitaka kununua magari, Serikali ililipia kwa asilimia 50 ya bei. Bei ya petroli ilikuwa karibu na bure, lita ililipiwa kwa Dola 0.4.....Hii iliwezekana kutokana na kudhibiti mafuta yatumike kwa manufaa ya wananchi wote na wageni wasubiri (MWENYE BOMBA HAKAI FOLENI)



2. Makazi ilikua ni haki ya msingi nchini Libya, Gaddafi aliwahi kusisitiza kwamba wazazi wake hawawezi kupata makazi hadi kila raia apate makazi/nyuma ya kuishi. Baba wa Gaddafi alifariki dunia wakati yeye na mama yake wakiwa wanaishi katika hema (kijijini kwao).




3. Wanandoa wote wapya nchini humo walipata Dola 50,000 (zaidi ya milioni 100 za madafu) toka Serikalini kwa ajili ya kununua makazi yao kuwasaidia kuanzisha familia mpya na Kila mwanamke aliyejifungua alipata posho ya Dola 5000 (zaidi ya milioni 10 za madafu)

                 

4. Alifanikiwa pia kufuta UJINGA miongoni mwa Walibya (asilimia 25 wa Walibya, wana shahada ya chuo kikuu). Wakati Gaddafi anachukua nchi asilimia ya waliokuwa na elimu ilikuwa 25, kwa sasa inafikia 83 na huenda ANGEUFUTA KABISAA UJINGA kwa njozi zake. Iwapo kuna waliokuwa hawawezi kupata huduma za elimu na afya wanazostahili, Serikali iliwalipia kwa ajili ya kuzipata nje ya nchi, hizi hazikuwa bure, walitakiwa kuchangia, walipata Dola2,300 kwa mwezi kwa ajili ya makazi na usafiri. Kwa waliomaliza vyuo, Serikali iliwapatia posho sawa na mshahara wa maofisa hadi watakapopata ajira yenye uhakika.



5. Kwa waliotaka kuwa wakulima, walipewa ardhi bure, nyumba katika shamba lao, vifaa, mbegu na mifugo kwa ajili ya kuanzisha miradi,


6. Kama hiyo haitoshi, alisimamia mradi mkubwa kabisa wa umwagiliaji, uliopewa jina la Great Man-made River, kuhakikisha maji yanakuwepo kwenye maeneo yote ya nchi yenye jangwa.


7. Wakati wa vikwazo kwa Serikali yake miaka ya 1980, Libya ilikuwa miongoni mwa nchi tajiri kabisa kwa msingi wa pato la ndani, ikiwa na kiwango cha juu cha maisha kuliko Japan. Ilikuwa ni nchi tajiri kuliko zote kabla ya vuguvugu la mapinduzi.




8. Huyu alikua mzalendo wa kweli mwenye njozi za kuikomboa Afrika nzima na kwa kuanzia alianza kushona vazi lenye PICHA ZA VIONGOZI NGULI AFRIKA akiwemo Mwalimu JK Nyerere.


9. Kuhusu mchango wa Gaddafi katika kuziondoa Serikali zote dhalimu Afrika na duniani kwa ujumla, alikuwa na chombo kinachoitwa Revolutionary Council Movement (RCM).Hii ni Kamati ya Vuguvugu la Mapinduzi. Gaddafi alijiona anao wajibu wa kusaidia vuguvugu la mapinduzi ili kusimika mataifa ambayo yatakuwa huru dhidi ya mataifa ya magharibi, Ulaya na Marekani. Kiongozi wake mkuu wa tawi la RCM-Tanzania, alikuwa Aman Nzugile Jidulamabambasi (marehemu).



10. Mwalimu aliwahi kumwambia Gaddafi kwamba pale kwake Butiama, anazungukwa na ndugu zake waislamu lakini hawana mahali pazuri pa kufanyia ibada, Gaddafi akajenga msikiti wa Butiama kulingana na idadi ya waumini wa kijiji cha Butiama. Baadaye Mwalimu akamwambia tena Gaddafi kwamba makao makuu ya chama chake na Serikali yake, Dodoma, hawana msikiti wenye hadhi ya makao makuu ya nchi. Gaddafi akajenga msikiti mkuu wa Dodoma.

11. Benki ya Afrika (BOA) na Kituo cha Redio na Televisheni cha Sauti ya Afrika (Voice of Afrika-VOA), vilianzishwa na utawala wa Gaddafi kutokana na ushauri huo wa Mwalimu. VOA ina idhaa ya Kiswahili, na watangazaji wa idhaa hiyo ni Watanzania na wachache kutoka Kenya.


​12. Gaddafi aliwaamini sana wanawake katika uongozi wake. alibaini kuwa wanawake wana jukumu kubwa zaidi ya kutunza nyumba na watoto. Imani yake (Gaddafi) inasemekana ni kuamini kuwa wanawake wangeweweza kuwa walinzi wake kwani isingekuwa rahisi kwa mwanaume wa Kiarabu kumpiga risasi na kumuua mwanamke. Wengine wamekuwa wakidai kuwa mapenzi ya Gaddafi kuwa karibu na wanawake warembo ndiyo yaliyomfanya aamini katika ulinzi ule wa Amazon Guards.​



Rais Barack Obama wa Marekani amewahi kusema: "Kosa baya zaidi katika urais wangu ni kukosa mpango wowote kwa ajili ya zama za baada ya kumuangusha Muammar Gaddafi nchini Libya."


Kwa mujibu wa kanali ya CNN, Barack Obama ametoa kauli hiyo katika mahojiano na Fox News akijibu swali kuhusu kosa kubwa alilowahi kufanya katika kipindi chake cha urais. Ingawa rais wa Marekani ametetea uingiliaji wa mgogoro wa Libya, lakini ameitaja hali ya hivi sasa nchini humo kuwa ni 'fedheha'. (http://kiswahili.irib.ir/uchambuzi/item/56302-)

Wosia wa Gaddafi kabla ya kifo 


KANALI Muammar Gaddafi, Mfalme wa Wafalme wa Afrika na mtu aliyekuwa na ndoto za kuliunganisha Bara la Afrika, sasa ameyeyuka katika ulimwengu huu, kama mshumaa uliowaka na kuteketea.


HUKU LICHA YA KUKUTWA KWENYE MTARO WA MAJI MACHAFU KABLA YA UMAUTI NA LICHA YA UTAJIRI LUKUKI ALIOKUWA NAO​,​ ALIKUFA AKIMUAMINI MUNGU


Katika sehemu ya wosia wake aliandika maneno haya


........ninaapa kwamba hakuna Mungu mwingine zaidi ya Allah na Muhammad ni Mtume wake, amani iko kwake. Ninaahidi nitakufa nikiwa Muislamu..............


Kanali Gaddafi pia aliwaasa wafuasi wanaomuunga mkono kuendelea kupambana. Alielezea msimamo wake kuwa amechagua kupambana hadi hatua ya mwisho na kufia katika ardhi ya Libya kuliko kuchagua njia nyepesi, ambayo kwa mtizamo wake, ni kitendo cha kujidhalilisha kisichokuwa na heshima, kukimbilia uhamishoni nje ya nchi yake, ambapo tayari alishapata ahadi nyingi za ulinzi.

�Iwapo nitauawa, nitapenda kuzikwa kwa mujibu wa taratibu za kiislamu, nikiwa nimevaa mavazi nitakayokuwa nimevaa wakati kifo changu kikitokea, bila mwili wangu kuoshwa, katika makaburi ya Sirte, jirani na familia na jamaa zangu.

No comments:

Post a Comment