Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, August 13, 2016

MBUNGE WA LUPEMBE AENDELEA NA ZIARA JIMBONI KWAKE


 WA KWANZA KUTOKA KUSHOTO NI DIWANI WA KATA YA KICHIWA PETER NYAHUYA WA KATIKATI NI MBUNGE WA JIMBO LA LUPEMBE JORAMU HONGORI NA WA TATU KUTOKA KUSHOTI NI KATIBU WA CCM VIJANA WILAYA YA NJOMBE

 WANANCHI WA IKANDO WAKIMSIKILIZA MBUNGE WAO

 MWENYEKITI WA SERIKALI YA KIJIJI CHA IKANDO  BWANA MWINAMI AKIFUNGUA MKUTANO MARA BAADA YA MBUNGE KUWASILI

 MBUNGE  WA LUPEMBE JORAMU HONGORI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA IKANDO



 Serikali  Imetenga Jumla Ya Shilingi Tririon 29.5  Kwaajili Ya Kuanzisha Miradi Mbalimbali Itakayo  wasaidia Wananchi Kufikia Uchumi Wa Kati Huku Asilimia 40 Zikienda Kwenye  Mipango  Ya Miradi Ya Maendeleo  Ya Afya,Umeme, Elimu Miundombinu.

Mbunge Wa Jimbo La Lupembe Joramu Hongori Akizungumza  Na Wananchi Wa Vijiji Vya Kata Ya Kichiwa  Ikando,Ibumila Na Kichiwa  Amesema Pia Serikali Imetenga  Kiasi Hicho  Cha Tririon 29.5 Kwaajili  Ya Uwekezaji Wa Viwanda ,Kuongeza Uzarishaji Kwenye Kilimo Katika Kipindi Cha Miaka Mitano.

 Hongori Amesema Mpango Wa Serikali  Katika Kilimo Ni Kushusha  Bei Ya Pembejeo Za Kilimo Ikiwemo Mbolea   Za Kwenye Maduka Ya Watu Binafsi  Na Zile Za Ruzuku Ili Kila Mkulima  Awe Na Uwezo Wa Kununua  Pembejeo Hizo Kwa Wakati Wake.

Amesema  Serikali Haitaweza Kuagiza Mbolea Kutoka Nje Ya Nchi Badala Yake Itachukuliwa Kwenye Viwanda Vya Ndani  Ya Nchi Huku  Wizara Ya Kilimo   Kwa Kushirikiana  Watafiti  Wa Udongo Wakiwa Na Jitihada Za Kutafiti Udongo Unaotakiwa Kwa Kilimo Na Kwamba Tayari Wamebaini Asilimia Kubwa Ya Udongo Unakosa Madini Ya Chokaa.

Awali Akimkaribisha Mbunge Huyo Diwani  Wa  Kata Ya Kichiwa Peter Nyahuya  Amewambia Wananchi Kusitisha Zoezi La Kuchimba Na Kumwaga Kifusi Kwenye Barabara  Iliyopo Kijijini Hapo  Kutokana Na  Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Kukubali Kwenda Kuwalimia Kwa  Mitambo Licha Ya Kuwa Haitamwagiwa Maji Na Kushindiliwa.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti Wa Kijiji Cha Ikando  Isack Mwinami  Amesema Pamoja Na Kijiji Hicho Kukabiliwa Na Uharibifu Wa Miundombinu Ya Barabara Lakini Pia Kuna Tatizo La Kukosekana  Kwa Huduma Za Maji  ,Uharifu Kuongezeka  Hususani Wizi Wa Mali Mbalimbali Na Kwamba Wanatarajia Kuanzisha Ulinzi Shilikishi Wakati Wowote Kuanzia Sasa.


No comments:

Post a Comment