Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, August 12, 2016

MAANDALIZI YA MAHAKAMA YA MAKOSA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI


mafi1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (kushoto) akiwa pamoja na wadau wengine wa Mahakama ya Tanzania walipotembelea kuangalia Maandalizi ya Jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama ya Rushwa na Uhujumu Uchumi lililopo kwenye Shule ya Sheria Sinza leo  jijini Dar es salaam. Baadhi ya Wadau wa Mahakama waliotembelea Mahakama hiyo ni Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Mawasiliano, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) 
mafi2
mafi3
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Kattanga (kulia) akiwaelezea jambo baadhi ya Makatibu Wakuu na watendaji wakuu wa Wizara na Taasisi za Serikali ambao ni Wadau wa Mahakama ya Tanzania walipotembelea kuona maendeleo ya Maandalizi ya Jengo litakalotumika kuwa Mahakama ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Sinza jijini Dar es salaam. Anayetazamana na Kattanga ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome na anayefuatia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Bibi Maimuna Tarishi.  
mafi4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Kattanga (kulia) wakiwaonyesha jambo wadau wengine wa Mahakama walipotembelea jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo jijini Dar esa salaam   
mafi6
mafi8
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (Kushoto) na Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Bibi Maimuna Tarishi wakizungumza jambo walipotembelea kuona maendeleo ya Maandalizi ya uanzishwaji wa Mahakama ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo Sinza jijini Dar es salaam

No comments:

Post a Comment