Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, July 6, 2016

WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU WA NJOMBE LEO WAMEUNGANA NA WAISLAMU WENGINE DUNIANI KOTE KUSHEREHEKEA SKUKUU YA EID ELFITR



Waumini Wa Dini Ya Kiislamu Mkoani Njombe Leo Wameungana Na Waumini Wengine Wa Dini Hiyo Duniani Kote  Baada  Ya Kutimiza Siku 29 Za Mfungo  Katika Kipindi Cha Mwezi Mtukufu  Wa Ramadhani Ambapo  Wametakiwa Kuendelea Kumucha Mungu Na Kutekeleza Masharti Ya Nguzo Kuu Tano Za Uislamu.

Rai Hiyo Imetolewa Na Imamu Wa Msikiti Mkuu Wa Njombe Mjini Rajab Msigwa  Wakati Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Mara Baada Ya  Waumini Kumaliza  Zoezi La Kuswali Na Kusema Kuwa Siku Ya Idd Ni Ya Kusherehekea  Na Siyo Siku Ya Kumuasi Mwenyezi Mungu  Wa Sulahana Watala Na Kwamba Wanasherehekea Uislamu Kwa   Kuwakalibisha Wengine Kujiunga Na Dini Hiyo.

Imamu Msigwa Amesema  Hategemei Muislamu Aliyefunga Kwa Siku 29 Akagundulika Akimkufuru Mungu  Kwa Kutenda Maovu  Nakwamba Waumini Hao Wanapaswa Kumucha Mungu Na Kuonesha Utii  Pamoja Na Kuwa Na Moyo Wa Kujitolea Na Kusaidia Wasiyo Jiweza Kwa Kutoa Sadaka Ili Kukuza Imani Ya Uislamu   Huku Wakitakiwa Kukemea Tabia Za Uharifu Wakati Wa Kusherehekea Skukuu Hiyo.

Amesema  Nguzo Tano Zinatakiwa Kutekelezwa Wakati Wa Mfungo Wa Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani  Ikiwemo  Kutoa Zaka,Kusimamisha Swala , Kuhiji Kwa Yule Mwenye Uwezo Wa Kwenda Kuhiji Na Kwamba Kufunga Katika Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani Ni Maandalizi Ya Kwenda Kuhiji Ambapo Kumaliza Sherehe Hizo  Wengine Wanapaswa Kuendeleza Siku Sita Za Kumalizia Mwezi Mtukufu Ramadhani.

Kwa Upande Wao Waumini Wa  Dini Ya Kiislamu  Wakizungumza Kwa Nyakati Tofauti  Akiwemo  Aman Mohamed  Gadau  Wametaka Jamii Kushirikiana Na Waumini Hao Kusherekea Skukuu Ya Eid Elfitr  Na Kuomba  Ulinzi Na Usalaama Kuimalishwa Kila Mahali  Huku Waumini Wakitakiwa Kuwalinda Watoto Wao  Kwaajili Ya Kujihadhari Na Matukio Ya Ajali  Na Uharifu Majumbani Mwao.

No comments:

Post a Comment