Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, July 26, 2016

WANANCHI WA ITULAHUMBA WILAYANI WANGING'OMBE MKOA WA NJOMBE WALIA NA UJENZI WA MADARAJA KWA MIAKA MINNE SASA .

                             NI YALE YA MTO IDEGE NA MTO MTITAFU.



 HAWA NI WANANCHI WA KITONGOJI CHA WANIKE WAKIWA NA MWENYEKITI WAO  KUCHIMBA UDONGO NA KUJAZA KWENYE GARI NA KUMWAGA KWENYE MASHIMO YA DARAJA HILO AMBALO MKANDARASI  HAKUKAMILISHA YAPATA MIAKA MINNE SASA.
 

 HILI NI GARI AMBALO LIMEKODIWA NA MDAU MMOJA WA KIJIJI CHA ISINDAGOSI JAMES MLIGO AMBAYE AMECHANGIA MILIONI TANO KWAAJILI YA KUJAZA KIFUSI KWENYE MADARAJA HAYO MAWILI KUWAUNGA MKONO WANANCHI HAO.

 HILI NI DARAJA LA MTO MTITAFU   AMBALO LINAUNGANISHA KATA YA ITULAHUMBA NA MDANDU  LINALOSAIDIA KUVUKA KWENDA SHULE YA SEKONDARI WANIKE.


WANANCHI HAO WAKICHIMBA KIFUSI KWAAJILI YA DARAJA LA MTO MTITAFU  BAADA YA KUKAMILISHA KUJAZA KIFUSI MTO WA KWANZA  WA IDEGE ULIOPO KIJIJI CHA ITULAHUMBA KITONGOJI CHA WANIKE INAYOUNGANISHA   KATA YA ITULAHUMBA NA MDANDU

 HILI NI DARAJA  LA MTO IDEGE AMBALO TAYARI LIMEKAMILIKA KUFUKIWA NA HAPA WANANCHI WANARUDI ZAO NYUMBANI KWAO




 HUYU NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE ANTONY  MAHWATA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSIANA NA MADARAJA  YANAYOLALAMIKIWA NA WANANCHI WA ITULAHUMBA NA KUSEMA KUWA MKANDARASI ALIYEKUWA AKITENGENEZA MADARAJA HAYO HAKUWA NA SIFA  ZA KUTENGENEZA NA HIVYO HALMASHAURI IKALAZIMIKA KUMSIMAMISHA NA KUMUWEKA MWINGINE WA KUKAMILISHA.
 MWENYE SUTI NYEUSI NI KAIMU MHANDIS WA UJENZI  WILAYA YA WANGING'OMBE MKOANI NJOMBE.




HILI NI JENGO JIPYA LA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE  NDIPO MAZUNGUMZO  BAINA YA VIONGOZI HAO NA WAANDISHI WA HABARI YALIFANYIKIA.

Na Michael Ngilangwa -Njombe

Baadhi ya Wananchi wa Kijiji Itulahumba Wilayani Wanging'ombe Wameitaka Halmashauri ya Wilaya Hiyo Kumchukulia Hatua za Kisheria Mkandarasi Aliyetelekeza Mradi wa Ujenzi wa Madaraja Katika Mito ya Mtitafu na Dege Yanayounganisha Vijiji Vya Kata Itulahumba na Mdandu.

Wakizungumza na Waandishi wa habari Wananchi  wa kijiji hicho Wamesema Ujenzi wa Madaraja Hayo Umetelekezwa Kwa Takribani Miaka Minne na Kusababisha Adha Kwa Wanafunzi na Wananchi Wanaotumia Barabara Hiyo Hasa Kipindi cha Masika Kutokana na Mito Hiyo Kujaa Maja na Kuharatisha Maisha Yao.

Kufuatia Adha Hiyo Wananchi Hao Wamamua Kuanza Ukarabati Katika Maeneo ya Madaraja Hayo Kwa Kumwaga Vifusi Kwa Nguvu Zao na Wadau wa Maendeleo wa Kata Hizo, Huku Wakiulalamikia Uongozi wa Halmashauri Hiyo Kwa Kushindwa Kukamilisha Ujenzi Huo.

Akitolea Ufafanuzi Kuhusu Ujenzi wa Madaraja Hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe Antony Mahwata Amesema Ujenzi Utakamilika Ndani ya Wiki Mbili, Huku Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri Hiyo Akielezea Hatua Walizochukua Baada ya Mkandarasi Kutelekeza Mradi Huo.

Aidha  Bwana Mahwata Amesema Halmashauri Hiyo Inatarajia Kukamilisha Ujenzi Wa Madaraja Hayo Ndani Ya Wiki Mbili  Kama Alivyomuahidi Mkuu Wa Mkoa  Wa Njombe  Na Kusema Wananchi Wa Itulahumba Wanatakiwa Kuwa Wavumilivu Wakati Matengenezo Yakifanyika Haraka  Kwani  Tayari Mkandarasi Amekwisha Kupatikana Wa Kukamilisha Madaraja Hayo Huku Akipongeza Wananchi Kwa Kazi Waliyoifanya Ya Kujaza Udongo Kwenye Eneo Hilo.

 Kaimu Muhandis Wa Ujenzi Wilayani  Wanging'ombe  Boniface Kasambo   Licha Ya Kutotoa Thamani Ya Madaraja Hayo  Lakini Amesema Halmashauri Imelazimika Kumusimamisha Mkandarasi  Wa Awali    Baada Yakuwa Hanauwezo Wa Kukamilisha  Miradi Hiyo  Ambapo  Sasa Wamempatia Mwingine Wa Kutekeleza Miradi Hiyo Aliyodai Imedumu Kwa Miezi Sita Na Siyo Miaka Miwili Iliyotwajwa Na Mwenyekiti Wa Halmashauri Huku Wananchi Nao Wakisema Ni Miaka Minne Sasa.

Hivi Karibuni Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi Aliuagiza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe Kuhakikisha Wanakamilisha Ujenzi wa Madaraja Hayo Ili Kuwaondolea Adha ya Miundombinu ya Usafiri Wananchi wa Itulahumba na Mdandu.  








No comments:

Post a Comment