Wednesday, July 27, 2016
MKUU WA WILAYA YA NJOMBE AMEZUNGUMZA NA WAUMINI WA KANISA LA TAG MELINZE
WAIMBAJI WA KWAYA YA TWENDE KWA NANI WAKITUMBUIZA
MCHUNGAJI WA KANISA LA TAG MELINZE CEFANIA TWEVE AKIZUNGUMZA NA WAUMINI WA KANISA HILO
HAPA MCHUNGAJI TWEVE MWENYE TAI UPANDE WA KUSHOTO ,ANAYEFUATA NI KATIBU TAWALA WILAYA YA NJOMBE JACKSON CHOTA ,WA TATU KUTOKA KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI,NA WA MWISHO NI ANNA WIKETYE KATIBU TAWALA MSAIDIZI WILAYA YA NJOMBE WAKIWA KWENYE KANISA LA TANZANIA ASSEMBLES OF GOD MELINZE LEO.
KATIBU TAWALA AKIZUNGUMZA WAKATI WA KUMKARIBISHA MKUU WA WILAYA
MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI AKIZUNGUMZA NA WAUMINI WA KANISA HILO
HAPA MCHUNGAJI ANAMSINDIKIZA MKUU WA WILAYA YA NJOMBE AKIWA NA BAADHI YA VIONGOZI ALIOONGOZANA NAO
Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Luth Msafiri Leo Ameanza Ziara Yake Ya Kutembelea Taasisi Za Serikali Na
Za Watu Binafsi Kwa Lengo La Kujitambulisha Akianza Na Makanisa 11 Ya Njombe Mjini Ambapo Akiwa Katika Kanisa La TAG Mkuu Huyo Wa Wilaya Ametaka Waumini Na Wananchi Kuwapuuza Baadhi Ya Watu Wanaoendekeza Siasa Kipindi Cha Kazi.
Kauli Hiyo Ameitoa Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Luth Msafiri Hii Leo Wakati Akizungumza Na Waumini Wa Kanisa La TAG Kwenye Kongamano La Wanaume Na Kusema Kuwa Siasa Zinakwamisha Maendeleo Kwa Jamii Hivyo Wanapaswa Kuepukana Na Wanaoendekeza Siasa Swala La Siasa Badala Yake Waongeze Juhudi Katika Uzarishaji Mali Na Kwa Manufaa Yao Na Taifa.
Aidha Bi.Msafiri Ameomba Waumini Wa Makanisa Mbalimbali Wilayani Njombe Kuendelea Kudumisha Amani Na Utulivu Ambayo Inategemewa Kuanzia Kwenye Makanisa Huku Akiomba Wachungaji Kuhimiza Waumini Kuacha Kuendelea Na Siasa Kwani Wametoka Kwenye Kipindi Kigumu Cha Uchaguzi Mkuu Wa Mwaka Jana.
Bi.Msafiri Amesema Chanzo Cha Amani Na Utulivu Ni Makanisa Hivyo Wachungaji Wanatakiwa Kutilia Mkazo Kuhubiri Amani Kila Siku Huku Akiomba Wananchi Na Waumini Kujenga Mazoea Ya Kuhudhuria Mikutano Inayoitishwa Na Viongozi Wa Serikali Ili Kupeana Utaratibu Na Mabadiliko Ambayo Wamejiwekea Au Kiongozi Wa Wilaya Ujumbe Atakaohitaji Kuwafikishia.
Kwa Upande Wake Mchungaji Wa Kanisa La TAG Melinze Cefania Tweve Amemshukuru Mchungaji Huyo Kwa Kuwatembelea Na Kutoa Ujumbe Huo Ambapo Ameahidi Kuufanyia Kazi Kwa Kuwaelimisha Waumini Kuhusiana Na Umuhimu Wa Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Serikali Na Kutaka Kumutegemea Mungu Zaidi Katika Kazi Zote Zinazofanyika.
Awali Akimkaribisha Mkuu Wa Wilaya Huyo Katibu Tawala Wilaya Ya Njombe Jackson Chota Alisema Ziara Hiyo Imelenga Kufahamiana Na Taasisi Mbalimbali Za Serikali Na Za Watu Binafsi Ili Mkuu Wa Wilaya Ashirikiane Vizuri Katika Kutekeleza Majukumu Ya Serikali Kwenye Halmashauri Yake Ya Njombe Na Kwamba Wakati Mwingine Atakuwa Anaongozana Na Wataalamu Wa Halmashauri Husika Kwenye Mikutano Ya Hadhara.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment