Tuesday, July 5, 2016
EWURA KUTANGAZA BEI ELEKEZI YA MAFUTA KESHO JULAI 6,IKIWA LEO WAKAZI WA NJOMBE WAMEKABILIWA NA UHABA WA MAFUTA KWA TAKRIBANI SAA TANO KITUO KIMOJA TU KILIKUWA KINATOA HUDUMA
NJOMBE
Mamlaka Ya Udhibiti Wa Nishati Ya Mafuta Na Maji Nchini EWURA Kesho Inatarajia Kutoa Bei Elekezi Kwa Wauzaji Wa Nishati Ya Mafuta Ambapo Wafanyabiashara Wa Mafuta Mkoa Wa Njombe Wameshauriwa Kutoficha Mafuta Kwa Lengo La Kusubiria EWURA Ipandishe Bei Kwani Kufanya Hivyo Ni Kukiuka Kanuni Na Sheria Za Biashara.
Rai Hiyo Imetolewa Na Afisa Biashara Wa Mkoa Wa Njombe Musa Lwalilino Wakati Akizungumza Na Uplands Fm Kuhusiana Na Tatizo La Kukosekana Kwa Mafuta Ya Petrol Katika Baadhi Ya Vituo Vya Mafuta Ambapo Kati Ya Vituo Saba Vya Mafuta Vilivyopo Njombe Mjini Ni Kituo Kimoja Cha Kwa Mwalabu Ndicho Kilichokuwa Kinaendelea Kutoa Huduma Kwa Wateja.
Bwana Lwalilino Amesema Kuwa Tatizo La Kukosekana Kwa Mafuta Njombe Mjini Kumetokana Na Meli Kuchelewa Kufikisha Mafuta Jijini Dar Es Salaamu Jambo Ambalo Limesababisha Msongamano Wa Magari Yanayokwenda Mikoani Na Matokeo Yake Ni Kukosekana Kwa Mafuta Maeneo Mbalimbali Ya Mikoa Nchini.
Aidha Lwalilino Amekemea Tabia Ya Baadhi Ya Wamiliki Wa Vituo Vya Mafuta Ambao Wanahifadhi Badala Ya Kuuza Kwaajili Ya Kusubilia Bei Elekezi Itolewa Na EWURA Na Kusema Kuwa Hatua Kali Zitachukuliwa Kwa Watakao Bainika Kukiuka Ikiwemo Kufutiwa Leseni Zao Za Biashara Na Kufikishwa Mahakamani Kujibu Tuhuma Zitakazokuwa Zinawakabili.
Akizungumza Na Uplands Fm Mkurugenzi Wa Kituo Cha Mafuta Chaugingi Ahamed Kaserehe Amesema Mafuta Yameadimika Kwa Siku Mbili Jijini Dar Es Salaamu Ambapo Yeye Alikuwa Na Mafuta Ya Ziada Ndiyo Anayoyauza Wakati Vituo Vingine Vikiwa Havina Mafuta Huku Akisema Kwa Mujibu Wa Leseni Ya EWURA Analazimika Kuuza Na Kuitaka Serikali Kufuatili Wauzaji Mafuta Ya Jumla Jijini Dar Es Salaamu Ili Kuondoa Adhaa Inayowakabili Wananchi.
Elika Mlope Ni Accountant Wa Kituo Cha Mafuta Gapical Amesema Wao Wameishiwa Tangu Jana Jioni Na Kuwahakikishia Wateja Kuwa Kufikia Mchana Wa Leo Yatakuwa Yamekwisha Wasili Njombe Na Huduma Kituo Hicho Kitaendelea Kutoa Huduma Ya Mafuta Ambapo Hadi Tunaingia Mitamboni Mafuta Yalikuwa Yameanza Kutolewa Kwa Baadhi Ya Vituo Vilivyokuwa Havitowi Mjini Njombe.
Diwani Wa Kata Ya Ramadhani Geoge Sanga Na Diwani Mstaafu Wa Kata Ya Imalinyi Enock Kiswaga Wakiwa Miongoni Mwa Wahanga Wa Kukosa Mafuta Wametaka Wafanyabiashara Wa Mafuta Kuweka Mafuta Ya Kutosha Huku EWURA Wakitakiwa Kufuatilia Baadhi Ya Wafanyabiashara Wanaosababisha Kukosekana Kwa Mafuta Kwa Makusudi Na Kuwachukulia Hatua Za Kisheria.
Awali Wakizungumza Kwa Nyakati Tofauti Wamiliki Na Madereva Wa Pikipiki Na Magari Walilalamikia Kukosekana Kwa Mafuta Kwa Muda Wa Masaa Takribani Sita Kutokana Na Mafuta Kucheloewa Kufika Jijini Dar Es Salaamu Baada Ya Meli Kuchelewa Kufikisha Ambapo Wameitaka Serikali Kuboresha Usimamizi Wake Kupunguza Kero Kwao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment