Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, May 7, 2016

VIONGOZI WA TAASISI MBALIMBALI WAKIWEMO WA SERIKALI WATAKIWA KUJENGA MAZOEA YA KUITISHA MIKUTANO YA WANANCHI NA KUFANYA VIKAO

 KAULI YA KATIBU TAWALA WILAYA YA NJOMBE JACKSON CHOTA AMBAYO AMEITOA WAKATI AKIWA MGENI RASMI KWENYE MKUTANO WA WALEMAVU WA VIUNGO
 MWENYEKITI WA WALEMAVU WA VIUNGO MBALIMBALI MKOA WA NJOMBE JACKSON FIHANGA

 HAWA NI BAADHI YA WAJUMBE WA KAMATI TENDAJI YA MKOA YA WALEMAVU MKOANI NJOMBE

Viongozi Wa Taasisi Za Serikali Na  Watu Binafsi Wilayani Njombe Wametakiwa Kuzingatia Kanuni Na Taratibu Za Utawala Bora Kwa Kuitisha Vikao  Kwa Mujibu Wa Sheria  Kwaajili Ya Kujadili Maendeleo Ya Usimamizi Wa Miradi  Inayotekelezwa Katika Maeneo Yao Ili Kuondoa  Migogoro  Ambayo Imekuwa Ikijitokeza  Hususani  Ile Inayohusu Maswala Ya Fedha.

Rai Hiyo Imetolewa Na Katibu Tawala Wilaya Ya Njombe Jackson  Chota Wakati Akizungumza Na Wajumbe Wa Kamati Tendaji Ya Walemavu Mkoa Wa Njombe  Ambayo Imekutana  Katika Ofisi Ya Chama Cha Walemavu Mkoa Kujadili  Maendeleo Ya Miradi Na Changamoto Zinazowakabili Walemavu Hao Pamoja Na Kushawishi Walemavu Wengine Walioko Nyumbani Kuwa Kitu Kimoja.

Katibu Tawala Chota  Amesema  Migogoro Mingi Huanzia  Kwenye Vipengele Vinavyo Husu Fedha  Baada Ya Wajumbe Na Wananchi Kutokuwa  Na Imani   Na Usimamizi Wake  NA kusababisha Kuwepo Kwa Masikitiko  Na Maneno Yenye Kulaumu Upande Wa Uongozi Kutokana Na Vikao Na Mikutano Kutoitishwa  Kwa Lengo La Kila Mmoja Kupewa Nafasi Ya Kuhoji Na Kushauri  Namna Wanavyoweza Kutekeleza Miradi.


Akisoma Risala Ya Chama Cha Walemavu CHAWATA Mkoa Wa Njombe Mwenyekiti Wa Chama Hicho Jackson Fihanga  Amesema Chama Hicho Kilianzishwa Mwaka 1982 Kufuatia Tangazo La Umoja Wa Mataifa  Kutangaza Kuwa Mwaka 1981 Ni Mwaka Wa Kimataifa Wa Walemavu  Na Serikali Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ililidhia  Tangazo Hilo Na Kuhimiza Kuanzishwa  Kwa Vyama Vya Walemavu.

Fihanga Amesema CHAWATA Njombe Imekuwa Ikishawishi  Walemavu Wengine Kuwa Pamoja,Kuwapa Ushauri Nasaha Walemavu Kuukubali Ulemavu Wao  Na Kuunda Matawi Katika Wilaya Na Vijiji Ambapo Chawata Na Chama Cha Wasiyoona Njombe  Vilifanikiwa  Kuanzisha  Mradi Wa Duka ,Kununua Gari Na Nyumba  Huku Kikishindwa Kupata Viongozi Wa Taifa Kutokana Na  Mkutano Wa  Uchaguzi Kutoitishwa.


Baadhi Ya Walemavu Mkoa Wa Njombe Wameiomba Serikali Kuingilia Kati  Kusimamia  Uchaguzi Wa Viongozi Wa Kitaifa Wa Walemavu  Na Kwamba Wamekuwa  Wakilalamikia  Kaimu Mwenyekiti Wa Chama Hicho  Ili Aitishe Mkutano Mkuu Wa Taifa  Wafanye Uchaguzi Wa Viongozi Wao Lakini  Amekuwa Hafanyi Hivyo.

No comments:

Post a Comment