Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, May 7, 2016

ACT WAZALENDO MKOA WA NJOMBE KUADHIMISHA SIKU YA KUTIMIZA MIAKA MIWILI JUMAMOSI IJAYO

 MWENYEKITI WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO MKOA WA NJOMBE ALLY MHAGAMA MARUFU SAGASAGA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI

 KAIMU KATIBU WA ACT MKOA WA NJOMBE NELSON KYANDO AKITOLEA UFAFANUZI JUU YA SIKU HIYO

Chama Cha ACT Wazalendo Mkoa Wa Njombe Kimelazimika Kuahirisha Sherehe Za Kutimiza Miaka Miwili Ya Kuanzishwa Kwa Chama Hicho  Mkoa Wa Njombe  Kutokana Na Sababu Mbalimbali Ikiwemo  Baadhi Ya Viongozi   Wa Chama Kuwa Na Majukumu Mengine Ambapo Kilele Cha Maadhimisho Hayo  Kitaifa Yanafanyika Mkuranga Mkoani Pwani.

Akizungumza Na Uplands Fm Mwenyekiti Wa Chama Cha ACT Wazalendo Mkoa Wa Njombe Ally Mhagama Maarufu Kama Sagasaga  Amesema  Chama Hicho Kwa Mkoa Wake Kinatarajia Kufanya Maadhimisho Hayo  Mnamo Mei 18 Mwaka Huu  Siku Ya Jumamosi Ya Wiki Ijayo Ambapo  Maadhimisho Hayo Yatakwenda Sambamba Na Uhamasishaji Wananchi Kuchangia  Damu Salama Kwaajili Ya Wagonjwa Wa Hospitali Ya Kibena.

Aidha Bwana Mhagama Amesema Jitihada Za Chama Hicho Kuhamasisha Wanachama Na Wananchi  Mkoa Wa Njombe Bado Zinaendelea  Kwani Wameanzisha Zoezi Hilo Baada  Ya Kutambua Uwepo Wa Changamoto Ya Kukosekana Kwa Damu Salaama Katika Hospitali  Zilizopo Nchini  Na Kuataka Wadau Wengine Kuunga Mkono Jitihada Zitakazofanyika Na Chama Hicho Za Kuchangia Damu Salaama.

Kwa Upande Wake Kaimu Katibu Wa Chama Cha ACT Wazalendo Mkoa Wa Njombe Nelson  Kyando Amesema Chama Hicho Kinatarajia Kuwafikia Wananchi Wa Maeneo Mbalimbali Yakiwemo Ya Vijijini  Ili Kuiambia Jamii Juu Ya Makusudio Ya Chama Hicho Juu Ya Kuhimiza Maendeleo Kwa Kila Mwananchi Pamoja   Na Kuongeza Idadi Ya Wanachama  Na Kwamba Chama Hicho Kitasikiliza Kero Zao.

Kyando Amesema Kwa Mujibu Wa Katiba Ya Chama Hicho   Wanatarajia Kupeleka Mahitaji Mbalimbali  Kwa Watu Wasiyojiweza  Kwa Kuwasaidia Mahitaji  Ya Msingi  Ili Kutoa Mfano Kwa Wananchi Na Wadau Wengine  Kujenga Mazoea Ya Kusaidia Makundi Hayo Yakiwemo Ya Wazee Huku Akitaja Misingi  Ya Katiba Ya Chama Hicho Kwani Miongoni  Ni Uwajibikaji  Na Usawa  Pamoja Na Uadilifu.

No comments:

Post a Comment