Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, May 10, 2016

TANWAT YAKABIDHI KISIMA CHA MAJI NA KUAHIDI KUCHANGIA MBAO ZAIDI YA MIA NNE KATIKA MTAA WA KIBENA HOSPITALI

 HAWA NI AKINA MAMA WA MTAA WA KIBENA HOSPITALI WAKISHEREKEA KUPATA KISIMA CHA MAJI

HAPA SASA WANAFURAHIA HUDUMA YA MAJI YA KISIMA KILICHOCHIMBWA NA KAMPUNI YA TANWAT NJOMBE

 KULIA NI AFISA UTAWALA WA TANWAT EDMUND MNUBI,WA PILI KUTOKA KULIA NI KAIMU MKURUGENZI WA KAMPUNI YA TANWAT  DKT RAJEEV SINGH NA WA TATU KUTOKA KULIA NI MENEJA MKUU WA MISITU KATIKA KAMPUNI HIYO ANTERY  KIWALE.



 AFISA MTENDAJI WA MTAA WA KIBENA HOSPITALI COLUMBA MSEMWA  AKISOMA TAARIFA FUPI KWA MGENI RASMI
 KULIA NI MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA KIBENA HOSPITALI WINFRED KAYOMBO,NA WA PILI KUTOKA KULIA NI DIWANI KATA YA RAMADHANI GEOGE MENSON SANGA


 HIKI NDIYO KISIMA AMBACHO KIMEKABIDHIWA KWA WANANCHI WA KIBENA HOSPITALI  NA KAMPUNI YA TANWAT NJOMBE





 MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA KIBENA HOSPITALI AKIWA NA DIWANI  WA KATA HIYO WAKIFURAHI NA KUPEANA MIKONO KWA KUFANIKISHA KUPATA KISIMA HICHO






 KAIM MKURUGENZI WA  TANWAT DKT RAJEEV  SINGH AKIWA NA AFISA UTAWALA WA KAMPUNI HIYO AKITOA HOTUBA YAKE











Mkurugenzi Wa Kampuni Ya  Tanwat Mjini Njombe   Dkt Rajeev Singh Ameahidi Kutoa  Msaada Wa Mbao

Zaidi Ya Mia Nne  Kwaajili Ya Kukamilishia Jengo La Ofisi Ya Serikali Ya Mtaa Wa Kibena Hospitali

Ambapo Amesema  Kampuni Hiyo Inatoa Misaada Endapo Wananchi Wataonesha Mfano  Wa Kuanza 

Utekelezaji  Wa Miradi Iliyopewa Kipaumbele.

Kaimu  Mkurugenzi Wa Kampuni Ya Tanwat   Dkt Rajeev  Singh Akitafsiliwa Lugha  Na Afisa Utawala Wa

Kampuni Hiyo  Edmund  Munubi Amepongeza   Serikali Ya Mtaa Wa Kibena Hospitali  Kwa Jitihada

Walizofanya Za Kuomba Kusaidiwa Kuchimbiwa Kisima Hicho  Ambapo  Kutokana Na Juhudi Za Wananchi

Walizoonesha   Ameahidi  KutoaMbao  Zaidi Ya Mia Nne Kwaajili Ya Ofisi Ya Serikali Ya Mtaa Huo.

Dkt Singh  Pia   Amekabidhi Mradi Wa Maji  Ya Kisima Kwa Uongozi Wa Mtaa Wa Kibena Hospitali

Uliogharimu Zaidi Ya Shilingi Milioni Mbili  Ambapo  Kukabidhiwa Kwa Mradi Huo  Kutasaidia Kutatua

Changamoto Ya Ukosefu Wa Maji Iliyokuwa Ikiwakabili Wakazi Wa Eneo Hilo Kwa Kipindi Cha Muda 

Mrefu.

Kwa Upande Wake  Meneja Mkuu Wa Misitu Wa Kampuni Ya Tanwat Antery Kiwale  Akizungumza Wakati

Wa Kukabidhi Mradi Huo  Amewataka Wananchi Kuonesha Ushirikiano Katika Kuilinda Misitu Ya

Kampuni Hiyo Kwa Kukemea Tabia Ya  Uchomaji  Hovyo Wa  Moto  Pamoja Na Kuwataja  Baadhi Ya Watu

Wanaojihusisha Na Wizi Wa Magogo Ya Mbao .

Diwani Wa Kata Ya Ramadhani Geoge Menson Sanga  Ameshukuru Wananchi Kwa Kujitokeza Kwa Wingi

Katika Kushiriki Ujenzi Wa Ofisi  Ya Mtaa Huo Ambapo Pia Amepongeza  Kampuni Ya Tanwat Kwa

Kuwakabidhi Kisima Hicho  Pamoja Na Ahadi Ya Kuwapatia Zaidi Ya Mbao Mia Nne Kwaajili Ya Jengo La

Ofisi Hiyo.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Serikali Ya Mtaa Wa Kibena Hospitali Winfred Kayombo Pamoja Na

Kushukuru Kwa Kukabidhiwa Mradi Huo Lakini Amesema Serikali  Itasimamia Matumizi Sahihi Ya Kisima

Hicho  Ili Wananchi Wanufaike Wote Kwa Kuwa Na Matumizi Mazuri Na Kisima Hicho Kidumu Kwa Muda

Mrefu.

Awali Akisoma Risala Fupi Mbele Ya Mgeni Rasmi Afisa Mtendaji Wa Mtaa Wa Kibena Hospitali Bi. 

Columba Msemwa  Amesema Katika Kutekeleza Mradi Wa Maji Ya Kisima  Hicho Wananchi  Wamechangia

Kiasi Cha Zaidi Ya Shilingi  Laki Mbili Huku Ujenzi Wa Jengo La Ofisi Wakichangia Zaidi Ya Shilingi milini

Sita  Na Fedha Nyingine Imepatikana Mfuko Wa Maendeleo Ya Kata  Ambapo Hadi Lilipofikia  Hatua Ya

Bimu Limegharimu Zaidi Ya Shilingi Milioni Tisa.

Wananchi Wa Mtaa Wa Kibena Washukuru Kwa Kukabidhiwa Kisima Hicho Ambacho Kimetajwa Kutatua

Changamoto Ya Kukosekana Kwa Huduma Za Maji Katika Mtaa Huo  Na Kuahidi Kuonesha Ushirikiano 

Mkubwa Kwa Kampuni Hiyo Kwani Imeonesha  Upendo Wa Kutosha Kwao.

No comments:

Post a Comment