Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, May 11, 2016

KIJANA MMOJA MKAZI WA IGAGALA WILAYA YA WANGING'OMBE AKUTWA AMEFARIKI LEO KATIKA KILABU CHA POMBE ZA KYENYEJI NJOMBE MJINI


 MWILI WA KIJANA MWENYE UMRI WA MIAKA 32  FIDELISI MHEPELA ULIPOKUTWA  ASUBUHI YA LEO KWENYE KILABU CHA POMBE ZA KYENYEJI CHA NDEVALONGE AMBAKO ALIKUWA ANALALA BAADA YA KUKOSA MAKAZI MJINI NJOMBE.



 BAADHI YA WANANCHI WAKIPANDA KWENYE GARI LA POLISI ILI KWENDA KUSAIDIA KUTOA MWILI HUO KUWEKA KWENYE CHUMBA CHA MAITI KIBENA ILI NDUGU ZAKE WAFIKE KUUCHUKUA KWAAJILI YA MAZISHI




 MASHUHUDA WAKIPANDA KWENYE GARI LA POLISI ASUBUHI YA LEO

 HUU NI MLANGO  WA CHUMBA CHA BIASHARA ALICHOKUWA AKILALA BAADA YA WATEJA KUONDOKA  ALIMOKUTWA MAREHEMU AKIWA AMEFARIKI DUNIA


Mkazi Mmoja Wa Kijiji Cha  Igagala Kata Ya Ulembwe Wilayani Wanging'ombe Fiderisi Mhepela Mwenye Umri Wa Miaka 32 Amekutwa Akiwa Amefariki Dunia Kwenye Kilabu Cha Pombe Za Kyenyeji  Cha Ndevalonge Kilichopo  Mtaa Wa Mpechi Eneo La Lutilage Mjini Njombe Ambapo  Mwili Wake Upelekwa Kuhifadhiwa Katika Chumba Cha Maiti   Cha Hospitali Ya Mkoa  Wa Njombe Ya Kibena.

 Wakizungumza Mapema Leo Baadhi Ya Wananchi Na Mashuhuda Wa Tukio Hilo  Wamesema  Mwili Wa Marehemu Fidelis  Mhepela  Umekutwa Asubuhi Ya Leo Ukiwa Chini Ya Sakafu  Ya Chumba Cha Biashara Ya Pombe Za Kyenyeji Ambacho Alikuwa Akilala   Kama Mlinzi  Baada Ya Kuomba  Kwa Wamiliki Kwamba Hana Sehemu Ya Kuishi  Huku Milango Yote Akiwa Amefunga .

Aidha Mashuhuda Hao Wamesema   Mara Nyingi Marehemu Alikuwa  Akilala Kwenye Chumba Hicho  Na Asubuhi Anaendelea Na Shughuli Za Kufanya Vibarua   Vya Kusomba Pombe Na Kwenda Kulima Kwa Watu Tofauti Tofauti  Na Kisha Jioni Anarudi Kujihifadhi Kwenye Kilabu Hicho  Ambacho Mauti Yake Ymemkuta Usiku Wa Kuamkia Leo  Pasipo Wafanyabiashara W    a Eneo Hilo Kufahamu Chanzo Cha Kifo Chake .

Kwa Upande Wake  Mwenyekiti Wa Serikali Ya Mtaa Wa Mpechi  Deogratias Msemwa Amethibitisha Kutokea Kwa Tukio Hilo Katika Mtaa Wake  Na Kusema Kuwa Chanzo  Cha Kifo Hicho Hakijafahamika  Ambapo  Jukumu La Kufanya Uchunguzi Wa Tukio Hilo Wameliachia Jeshi La Polisi  Litakalo Toa Taafira Ya Kifo Hicho Baada Ya Kupata Taarifa Ya Daktari.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Limefika Kwenye Tukio Hapo Kwa Wakati Ili Kuimarisha  Ulinzi Na Usalaama     Na Kuchakua Mwili   Wa Kijana Huyo  Kwaajili Ya Kuhifadhi Kwenye Chumba Cha Maiti Kibena Huku Uchunguzi Wa Tukio Hilo Ukiendelea.

No comments:

Post a Comment