Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, May 13, 2016

SSRA YATOA SEMINA KWA WAKULIMA MKOA WA NJOMBE KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI YA TAIFA YA JAMII ILIYOPO KARIBU NAO

 MRAJISI WA VYAMA VYA USHIRIKA MKOA WA NJOMBE EXAUD SAPALI BAADA YA KUWASILI UKUMBI WA SEMINA AKIWA MGENI RASMI KWENYE SEMINA HIYO YA SSRA LEO


MWENYEKITI WA CHAMA CHA USHIRIKA MKOA WA NJOMBE  NJORECU  CLEMENCE MALEKELA AKIMKARIBISHA MGENI RASMI AWEZE KUZUNGUMZA NA WAKULIMA HAO



 MWEZESHAJI  WA SEMINA KUTOKA  SSRA MAKAO MAKUU DAR ES SALAAM BI.  SARAH  KIBONDE MJULA
 MRAJISI  WA VYAMA VYA USHIRIKA MKOA WA NJOMBE EXAUD SAPALI NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA USHIRIKA MKOA WA NJOMBE  CLEMENCE MALEKELA WAKITETA JAMBO KABLA YA KUANZA KWA SEMINA



 MRAJISI AKIWA MGENI RASMI KWENYE SEMINA YA LEO





 PICHA YA PAMOJA  NA WAKULIMA WALIOHUDHURIA SEMINA HIYO LEO NJOMBE






















Mamlaka Ya Usimamizi Na Udhibiti Wa Sekta Ya  Hifadhi  Ya Jamii Imewataka Wakulima,Wafanyabiashara Na Wananchi  Kujiunga Na Mifuko Ya Taifa Ya Hifadhi Ya Jamii Iliyopo Hapa Nchini  Ili Waweze Kunufaika  Na Mafao Ya Uzeeni  Pamoja Na Kupatiwa Mikopo  Ya Kuendeshea Shughuli Zao  Za Kiuchumi Kwa Wanaohitaji Mikopo.

Akizungumza  Wakati Wakufanga Semina Ya Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii  Kwa Shirikisho La Wakulima Mkoa Wa Njombe,  Mrajisi Wa Vyama Vya Ushirika  Exaud Sapali  Ametaka  Wananchi Kujiunga Na Mifuko Ya Hifadhi Ya Jamii Kwaajili Ya Kunufaika Na  Matibu Bure Katika Hospitali  Na Vituo Vya Afya  Pamoja Na  Kupata Mafao   Ya Uzeeni  Watakayopata  Wakistaafu Kazi.

Aidha  Bwana Sapali  Pia Ametaka Wakulima Hao Kujiunga Na Vyama Vya Ushirika  Vilivyopo Kwenye Maeneo Yao   Ambavyo Vitakuwa Vinawasaidia Kuwakopesha Mikopo  Yenye Riba Nafuu  Kwaajili Ya Kuinua Uchumi Wa Kila Mmoja  Huku Akisema Serikali Imekwisha Fufua Chama Cha Ushirika Cha Mkoa Wa Njombe  NJORECU Kinachounganisha  Halmashauri Zote Ambacho Kilitelekezwa Tangu Mwaka 1994.

Akitoa Semina Ya Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii Kwa Shirikisho La Wakulima Mkoa Wa Njombe  Mkurugenzi Wa Mawasiliano Na Uhamasishaji  Wa Mamlaka Ya SSRA    Bi. Sarah Kibonde Mjula  Amesema Kuna Mifuko Saba Ya Hifadhi Ya Jamii Ambayo Ilianzishwa Na Serikali Kwa Lengo La Kukabiliana Na Majanga  Mbalimbali  Yatakayojitokeza  Huku Akizitaja Nguzo Kuu Tatu Na  Kuzifafanua Zaidi .

Wakizungumza Na Uplands Fm Mara Baada Ya Semina Hiyo Baadhi Ya Wakulima Wameshukuru  Kwa Kupatiwa Elimu Ya Kujiunga Na Mifuko  Mbalimbali Ya Hifadhi Ya Jamii  Na Kuahidi Kujiunga Kwani  Wametambua Umuhimu Wa Mifuko Hiyo Huku Wengine  Wakiwa Na Hofu Kwa Kufikisha  Matatizo  Yao Yakitokea Baina Ya Mifuko Hiyo  Kutokana Na Ofisi Za SSRA Kuwa Dar Es Salaamu Kama Ofisi  Nyingine.

Clemence Malekela Ni Mwenyekiti Wa Chama Cha Ushirika Mkoa Wa Njombe NJORECU  Amewashukuru Wakulima Hao Walioshiriki Semina Hiyo   Kwani Wamepata Elimu Ya Kutosha Juu Ya Umuhimu Wa Vyama Vya Ushirika Na  Kujiunga Na Mifuko Ya Taifa Ya  Hifadhi Ya Jamii Na Kutaka Kuwashawishi Wakulima Wengine Kujiunga Na Vyama Vya Ushirika Vilivyopo Karibu Nao Ili Waunganishwe Na Mifuko Ya Hifadhi Ya Taifa Ya Jamii  .

No comments:

Post a Comment