STAKABADHI HIZO NI HIZI AMBAZO UNAZIONA APA
HAWA NI MADEREVA WA BODABODA WALIPOKUWA KWENYE KIKAO KIFUPI
PIA WAMELALAMIKIA KUOMBWA RUSHWA NA BAADHI YA WAFANYA KAZI WA WAKALA HUYO
STAKABADHI HIZI HAZINA HATA MIHURI YA KAMPUNI HUSIKA
HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE IMEPIGA MARUFUKU WANANCHI KUTOA FEDHA NA KUKATIWA STAKABADHI KAMA HIZI LAKINI YASHANGAZA BADO ZINAENDELEA KUTOLEWA NA MAWAKALA
HAWA NI MADEREVA WA PIKIPIKI MAARUFU KAMA BODABODA
Wamiliki Na Madereva Wa Pikipiki Maarufu Kama Bodaboda Mjini Njombe Wameitupia Lawama Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Na Mamlaka Zinazohusika Na Usimamizi Wa Tozo Za Vyombo Vya Moto Ambazo Bado Stakabadhi Zake Zinatolewa Zilizoandikwa Kwa Mkono Licha Ya Halmashauri Hiyo Kupiga Marufuku Stakabadhi Hizo.
Wakizungumza Kwenye Kikao Kifupi Kilichowakutanisha Madereva Wa Pikipiki Katika Uwanja Wa National Housing Wamesema Licha Ya Halmashauri Hiyo Kutangaza Kwamba Stakabadhi Zinazotakiwa Kutolewa Na Mamlaka Zote Zinazohusika Na Uchangishaji Wa Fedha Na Mapato Ya Halmashauri Ziwe Za Kwenye Mashine Za Kielectronic Lakini Bado Wanapewa Zilizoandikwa Kwa Mkono.
Aidha Madereva Hao Wamekosoa Mpango Wa Mawakala Waliowekwa Na Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Wa Kuwapatia Stakabadhi Zilizo Andikwa Michango Ya Ushuru Wa Mazao Na Misitu Ikiwa Wao Hawauzi Mazao Wala Mbao Za Misitu Jambo Lililosababisha Kukosa Imani Na Mawakala Wanaochukua Tozo Za Maegesho Kuwa Huenda Zikawa Zinaishia Mifukoni Kwa Watu Wachache.
Katika Hatua Nyingine Madereva Hao Wamelilalamikia Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Kwa Kushindwa Kutekeleza Agizo La Mkuu Wa Jeshi La Polisi Wilaya Ya Njombe OCD Msolo Hamisi Msolo Alilotoa Siku Ya Kikao Baina Ya Madereva Bajaji,Madereva Daladala Na Madereva Wa Pikipiki, Agizo Ambalo Lilikemea Tabia Ya Watu Wasiyo Maafisa Usalama Wa Barabarani Kujihusisha Na Ukamataji Wa Vyombo Vya Moto.
Akizungumza Mbele Ya Madereva Hao Mwenyekiti Wa Madereva Wa Bodaboda Wilaya Ya Njombe Filemon Mwinuka Ameunga Mkono Malalamiko Ya Madereva Hao Kwa Kusema Wamekuwa Wakinyanyasika Na Kuyumbishwa Na Watu Wanaojiita Mawakala Ambao Wamekuwa Wakikamata Pikipiki Na Magari Madogo Aina Ya Tax Kwaajili Ya Maegezo Ikiwa Wao Hawana Utalaamu Wowote Wa Kukamata Vyombo Vya Moto.
Bwana Mwinuka Ametaka Pia Madereva Hao Kufuata Sheria Na Kanuni Za Usalaama Wa Barabarani Kwa Kuacha Kubeba Abiria Zaidi Ya Mmoja,Kuvaa Kofia Ngumu Kila Anapoendesha Pikipiki Huku Kampeni Ya Kukamata Baadhi Yao Wanaokiuka Taratibu Zilizoanishwa Na Maafisa Usalama Wa Barabarani Na Sumatra ikiendelea Kwaajili Ya Usalaama Wa Mwendeshaji Mwenyewe.
Siku Chache Zilizopita Ilimunukuu Afisa Habari Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Yasinta Kisima Akisema Wananchi Hawatakiwi Kutoa Pesa Ya Aina Yoyote Ile Kwa Watendaji Na Mawakala Watakao Chukua Fedha Na Kutoa Stakabadhi Zilizoandikwa Kwa Mkono Huku Jeshi La Polisi Nalo Lilitoa Agizo Kwamba Haruhusiwi Mtu Yeyote Kukamata Vyombo Vya Moto Ambaye Siyo Afisa Usalama Wa Barabarani Agizo Ambalo Limeonekana Kupuuzwa Na Baadhi Ya Mawakala.
No comments:
Post a Comment