Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, May 8, 2016

JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE LA WATAKA WANANCHI KUIMARISHA ULINZI SHIRIKISHI



Wananchi Mkoani Njombe Wametakiwa Kuimarisha Vikosi Vyao Vya Ulinzi Shirikishi Na Kuonesha Ushirikiano  Kwa Viongozi Waliopo Karibu Nao Na Kwa Jeshi La Polisi Pindi Wanapogundua Kuna Watu Wanaotiliwa Mashaka  Katika Maeneo Yao Ili Kuwalia Doria Kwaajili Ya Kuepusha Matukio Ya Uvunjifu Na Uharifu Kwa Jamii.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Kamanda Wa Jeshi La Polisi Mkoa Wa  Njombe Pudensiana Plotas  Wakati Akizungumza Na Uplands Fm Kuhusiana Na Namna Jeshi Hilo Lilivyo Jipanga Kuhakikisha Matukio Ya Uharifu Hayaendelei Kwa Kasi Ambapo Amesema Doria Zimeendelea Kufanyika Kila Mahala  Na Kutaka Wananchi Kushirikiana Kwa Pamoja Kutokomeza  Vitendo Hivyo.

Aidha Kamanda Plotas Amesema Jeshi La Polisi Bado Linaendelea Na Msako Wa Kuwabaini Waharifu Waliosababisha Matukio Mawili Ya Mauaji Katika Mtaa Wa Idundilanga Na Ngaranga Kwenye Shule Ya Sekondari Wende  Na Kuzuia Waharifu Wengine Ambao Wanatarajia Kufanya Matukio Na Kuimarisha Taarifa Za Kiiteligensia Kubaini Wahusika Waliko.

Hata Hivyo Ameshauri Wakulima Na Wafanyabiashara  Wa Mkoa Wa Njombe Kuzitumia Zaidi Taasisi Za Kifedha Kuhifadhi Pesa Zao  Pindi Wanapouza Mazao Yao  Huku Akisema Wafanyabiashara Wanatakiwa Kuzingatia Muda Wa Kuuza Biashara Zao Kwa Kutouza Hadi Usiku Wa Manane  Ili Kuwaepusha Na Matukio  Yanayoweza Kujitokeza Ya Uvunjifu Wa Amani.

Baadhi Ya Wananchi Mjini Njombe Wameomba Jeshi La Polisi Kufanya  Doria  Shemu Mbalimbali  Zikiwemo Za Vyombo Vya Usafiri Kukagua Silaha  Na Watu Wanaokwenda  Kufanya Uharifu Sehemu Frani Kwani Matukio Ya Mauaji Yanayofanywa Na Majambazi Yanatokana Na Jeshi La Polisi Kushindwa Kukagua Mizigo Ya Abiria Wanaosafiri Kwenye Mabasi Na Magari .

No comments:

Post a Comment