Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, March 22, 2016

MWILI WA MAREHEMU SARAH DUMBA AMBAYE ALIKUWA MKUU WA WILAYA YA NJOMBE WAHIFADHIWA HOSPITALI YA ILEMBULA


Saraha Dumba

 MAREHEMU SARAH DUMBA  ENZI  ZA UHAI WAKE  ALIPOKUWA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI OFISINI KWAKE KUHUSIANA NA  WAKULIMA KUONGEZA KASI YA KILIMO CHA CHAI NJOMBE IGOMINYI.
 MKUU WA MKOA WA NJOMBE  DKT REHEMA NCHIMBI AKIZUNGUMZA  HII LEO OFISINI KWAKE JUU YA KIFO CHA MKUU WA WILAYA YA NJOMBE  MAREHEMU SARAH DUMBA
 
 BAADA YA KUPATWA NA HALI YA KUKOSA HEWA NA KUTAPIKA  MAREHEMU ALIPELEKWA KATIKA HOSPITALI YA KIBENA NJOMBE KWA MATIBABU NA NDIPO ALIPOGUNDULIKA AKIWA AMEFARIKI DUNIA



MCHUNGAJI WA KANISA LA TAG TANZANIA ASSEMBLES OF GOD CEFANIA TWEVE AKIWA NYUMBANI KWA MAREHEMU AKIONGEA NA WAANDISHI WA  HABARI



EDWIN KILASI  ALIKUWA KATIBU WA  UHAMASISHAJI WA MAJI NYENGA AMEMUELEZEA  MAREHEMU SARAH DUMBA KWAMBA NI MIONGONGI MWA VIONGOZI WALIOSHIRIKI KUHAMASISHA  UCHANGIAJI WA MRADI WA MAJI NYENGA YASOGEZWE NJOMBE MJINI KWA KUCHANGIA ELFU 30 KILA MMOJA MWENYE MAPENZI MEMA.
.......................................................................................................................................................................

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi Ameelezea Kifo cha Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Njombe Marehemu Sara Dumba Aliyefariki Jana Usiku Katika Hospitali ya Mkoa Huo (Kibeana) Wakati Akipatiwa Matibabu Baada ya Kuugua Ghafla.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini Kwake Dkt. Nchimbi Amesema Mwili wa Marehemu Utasafirishwa Kwenda  Jijini Dar Es Salaam Kwa Ajili ya Mazishi, na Kwamba Kabala ya Kusafirishwa Mwili wa Marehemu Sara Dumba Utapelekwa Katika Kanisa la KKKT Mjini Njombe Kwa Ajili ya Misa ya Mazishi.

Nao Baadhi ya Wananchi , Viongozi wa Dini, Serikali na Siasa Waliozungumza na Upland's Redio Wameelezea Namna Walivyokuwa Wakishirikiana na Marehemu Wakati wa Uhai Wake Katika Kutekeleza Miradi ya Maendeleo Pasipo Kujali Itikadi Zao.

Kabla ya Kuteuliwa Kushika Wadhifa wa Ukuu wa Wilaya  Marehemu Sara Dumba Alikuwa Mtangazaji wa Shirika la Habari Tanzania Kipindi Kili Ilijulikana Kama Redio Tanzania Dar Es Salaam (RTD).

Mungu Alitoa na Mungu Ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe, Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Ma Hali Pema Peponi , Amen

No comments:

Post a Comment