Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, March 24, 2016

JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE LAJIPANGA SAWASAWA KUKABILIANA NA UHARIFU MSIMU WA SKUKUU YA PASAKA

 KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE PLODENSiANA PLOTAS  AKIZUNGUMZA  NA WAANDISHI AKIWA OFISINI KWAKE




Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Limesema Limejipanga Kikamilifu Kudumisha Amani Na Utulivu Kwa Kukabiliana Na Uharifu  Mbalimbali Utakaojitokeza Katika Kipindi Hiki Cha Skukuu Ya Pasaka  Kwa Kuimarishila  Ulinzi Katika Ofisi Za Serikali Na Za Watu Binafsi Bila Kusahau Maeneo  Ya Nyumba Za Ibada.

Akizungumza Na Uplands Fm Radio Kamanda Wa Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Plodensiana Plotas Amewataka Wananchi  Kusherekea Skukuu Kwa Amani Na Utulivu  Pasipo Kuibua Vurugu Mbalimbali   Zinazoweza Kuhatarisha Usalama Wa Eneo Husika  Na Kutaka  Serikali Za Mitaa Na Vijiji Kuonesha Ushirikiano Kwa Kutoa Taarifa.

Aidha Kamanda Plotas Amewataka Wamiliki Na Madereva Wa Vyombo Vya Moto Kuwa Makini Siku Ya Skukuu  Wakiwa Barabarani Kwa Kuacha Kutumia Vileo Vya Aina Yoyote Ile  Ambapo Jeshi La Polisi Limesema Halitasita Kuwachukulia Hatua Kali Za Kisheria Kwa Wale Wote  Watakaokamatwa Kuhusika  Wakiendesha Chombo Cha Moto Wakiwa Wamelewa Pombe.

Amesema     Jamii  Inatakiwa Kuondoa Imani Za Kufanya Matukio Ya Uharifu Msimu Wa Skukuu  Kwa Kulewa,Kuvunja Nyumba Na Kufanya Uharifu Wa Kuiba Mali  Ambapo Ametaka  Wananchi Kupiga Simu  Ya Kamanda Wa Polisi  Ya 0754061979  Ili Jeshi La Polisi Liweze Kufika Eneo La Tukio  Na Kufanikisha Kuimarisha Usalaama.

Kwa Upande Wake  Baadhi Ya Wananchi Mjini Njombe Wameomba Watumiaji Wa Vyombo Vya Moto Kuwa Makini Wakiwa Barabarani  Na Kusema Kuwa Vyombo Vinavyosimamia  Usafirishaji  Abiria  Kuchunguza Baadhi Ya Madereva Ambao Wamekuwa Wakipandisha Nauli Msimu Wa Skukuu  Na Wengine Kuchukua Abiria Wanaofika Mbali  Na Wa Jirani Kuachwa.

No comments:

Post a Comment