Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, January 3, 2016

WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI AINA YA MAWE WA KUTOKA MTAA WA SIDO MJINI NJOMBE WAMELAZIMIKA KWENDA OFISI YA MADINI MKOA KUPATA HATIMA YAO YA KUPEWA LESENI YA MACHIMBO


 WACHIMBAJI HAO WAKIWA KATIKA OFISI ZA MADINI  MKOA WA NJOMBE




 MJIOLOJIA KUTOKA OFISI YA MADINI MKOA WA NJOMBE  BWANA JOHN MAGANGA AMESEMA KWAKUWA HAWAJAFIKIA MWAFAKA  WACHIMBAJI HAO NA SERIKALI YA MTAA YAKWAMBA NANI WAKUMILIKI LESENI HATAKIWI KUONEKANA  MTU YEYOTE AKIGONGA MAWE ENEO HILO.





 VIONGOZI WA SERIKALI YA MTAA WA SIDO WAKIRUDI NYUMBANI KWAO BAADA YA KUMALIZA KIKAO KATIKA OFISI ZA MADINI





Sakata La Wachimbaji Wadogo Wa Madini Aina Ya Mawe  Wa Ganga Lyandefu  Limeingia Dosari Baada Ya Wachimbaji Hao  Kushindwa Kufikia Mwafaka    Ya Nani Amiliki Leseni Ya Machimbo  Ya Madini Kati Ya Serikali Ya Mtaa Na Kikundi Cha Wachimbaji  Cha Jua Kali  Hali Iliyosababisha Ofisi Ya Madini Kufungia Eneo Hilo Kuanzia Jana.

Akizungumza Na Waandishi Mjiolojia Kutoka Ofisi Ya Madini  Mkoa Wa Njombe John Maganga  Amesema Eneo Hilo La Machimbo Ya Ganga Lyandefu  Halitakiwi Kuendelea Na Shughuli Za Uchimbaji Wa Madini Ya Mawe  Kutokana Na Kikundi Cha Wachimbaji Wa Eneo Hilo Kushindwa Kufikia Mwafaka Na Serikali Ya  Eneo Hilo   Yakwamba Nani Amiliki Leseni Ya Machimbo Hayo.

Aidha   Maganga  Amesema Ofisi Ya Madini Haina Tatizo  Na Mmiliki Wa Leseni  Na Kwamba  Mtu Yeyote Anaweza Kumiliki  Isipokuwa Makubaliano Ya Wamiliki Wa Eneo La Madini Yanatakiwa Yawepo Ndipo Ofisi Hiyo Itowe Leseni   Ambapo  Wachimbaji Wa Madini Aina Ya Mawe Mtaa Wa Sido Kushindwa Kufikia Mwafaka  Wanalazimika Kufungia Eneo Hilo Kwa Muda Usiyojulikana.

Wakizungumza Wakiwa Katika Ofisi Ya Madini Mkoa Wa Njombe  Wanakikundi Cha Uchimbaji Madini Ya Mawe  Jua Kali Cha  Eneo La Ganga Lyandefu   Katika Mtaa Wa Sido  Wamesema Hawajaridhishwa Na Majibu Yaliotolewa Na Ofisi Ya Madini  Pamoja Na Maamuzi Ya Serikali Ya Mtaa  Wa Sido  Ambapo Wameiomba Ofisi Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Kuingilia Kati Sakata Hilo.

Wamesema Kutokana Na Maamuzi Hayo  Wao Kama Wachimbaji  Wa Eneo Hilo   Wataendelea Na Shughuri Za Uchimbaji   Kama Kawaida  Hadi   Serikali Ipeleke Jeshi La Polisi Liwapige Na Mabomu  Lakini Wao Wataendelea Kufuatilia Ngazi Za Juu Kuanzia Diwani, Mkuu Wa Wilaya  Na Mkuu Wa Mkoa .

Ray Mond Mbuligwe  Ni Mwenyekiti Wa Kikundi  Cha Wachimbaji Madini Ya Mawe Katika Eneo La Ganga Lyandefu  Cha Jua Kali  Amesema Kikao Hicho Hakija Zaa Matunda Kwani Wachimbaji Hao Wameshindwa Kuridhika Na Majibu Ya Kwenye Kikao Hicho.

Mtandao Huu Umemtafuta Kwa Njia Ya Simu Mwenyekiti Wa Serikali Ya Mtaa Wa Sido  Kutolea Ufafanuzi Juu Ya Hatima Ya  Kikao Kilichofanyika Katika Ofisi Za Madini Mkoa Wa Njombe  Kikiwa Na Lengo La Kuafikiana Juu Ya Machimbo Hayo Richard Bimbiga   Amesema Hawezi Kuzungumza Chochote Kutokana Na Kuchoka Kwa Kuwa Alikuwa Kwenye Kikao Kwa Muda Mrefu.


No comments:

Post a Comment