PROF. MUHONGO ATAKA TANESCO KUSHIRIKIANA NA WAZALISHAJI WADOGO
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akimsikiliza
Mkurugezi Mkuu wa Kampuni ya Kufua umeme kwa kutumia mabaki ya miti aina
ya Miwati na kampuni ya kuzalisha nguzo za umeme , TANWAT, Dkt. Singh
Rajeer (wa nne kulia) wakati alipotembelea kampuni hiyo katia ziara yake
ya kutembelea miradi ya umeme Mkoa wa Njombe. Wengine katika picha (wa
pili kushoto) ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sarah Dumba, wa kwanza kulia
ni Katibu Tawala, Mkoa wa Njombe, Jackson Saitabahu (wa kwanza kulia) na
wa pili kulia ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Ziwa Nyasa,
Mhandisi Fred Mahobe.
Meneja
wa Kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji katika Bwawa la Kihansi,
Mhandisi Pakaya Sakaya (Wakwanza kulia)akimweleza jambo Wazriri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo (katikati), wakati wa ziara
ya kikazi ya kukagua miradi ya umeme katika kituo cha kufua umeme cha
Uwemba, nje kidogo ya mji wa Njombe. Kwa mujibu wa Mhandisi Pakaya,
Bwawa hilo lina uwezo wa kuzalisha kilowati 843. Wa kwanza kushoto mbele
ni ni Katibu Tawala, Mkoa wa Njombe, Jackson Saitabahu.
Waziri
wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo akimsikiliza Sister Imaculata
Mdoe wa Shirika la Wabenedictin Njombe ( kushoto kwake) wakati wa ziara
ya Waziri katika bwawa la kufua umeme la Uwemba. Katika risala yake
Sister Imaculata alimweleza waziri ombi la serikali kusaidia ujenzi wa
bwawa linalomilikiwa na Shirika hilo katika eneo hilo ambalo litakuwa na
uwezo wa kuzalisha kilowati 317 za umeme kwa kutumia maji na uwezo wa
kuhudumia vijiji vinne.
Mkuu
wa Wilaya ya Njombe, Sarah Dumba (katikati) akimweleza jambo Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo wakati wa ziara yake. Aidha,
katika ombi lake kwa Waziri, Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza umuhimu wa
Shirika la Wabenedictin kusaidiwa ili waweze kutekeleza mradi wao wa
kuzalisha umeme kwa kutumia maji katika eneo la Uwemba nje kidogo ya mji
wa Njombe, kutokana na umuhimu na mahitaji yake kwa jamii inayotarajiwa
kunufaika na mradi huo.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo na uongozi wa Mkoa wa
Njombe, akiwemo pia Mbunge wa Njombe Mjini Edward Mwalongo wakifanya
majumuisho ya ziara yao nje ya kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia
maji katika bwawa la Uwemba mara baada ya kutembelea miradi kadhaa ya
kufua umeme katika Mkoa huo.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo akisaini kitabu cha
wageni mara baada ya kuwasili katika kampuni ya kufua umeme kwa kutumia
mabaki ya miti aina ya Miwati na kampuni ya kuzalisha nguzo za umeme ya
TANWAT. Wanaoshuhudia ni baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo na ujumbe
uliongozana na waziri katika ziara hiyo.
Waziri wa Nishati na Madini, Prof.
Sospeter Muhongo ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kufanya
majadiliano na Kampuni ya Kufua Umeme kwa kutumia mabaki ya miti ya
Miwati ya TANWAT, ili kampuni hiyo iongeze kiwango cha uzalishaji umeme
kutoka Megawati 2 zinazozalishwa sasa kufikia megawati 10.
Agizo hilo linafuatia ziara ya Waziri aliyoifanya katika kampuni hiyo ikiwa ni ziara yake ya kikazi kutembelea miradi ya umeme katika Mkoa wa Njombe, ambapo Meneja Mkuu wa Misitu wa kampuni hiyo, Antery Kiwale amemweleza , Prof Muhongo kuwa, kampuni hiyo ina uwezo wa kuzalisha megawati 2.5 na kutumia megawati 1.4 kwa matumizi ya kiwanda na kiasi cha megawati 0.6 kinauzwa kwa TANESCO.
Aidha, Prof. Muhongo amewataka TANESCO kubadilika kiutendaji ili kuongeza wigo wa uzalishaji umeme kwa kuwatumia wazalishaji wakubwa, kwa kati na wadogo ambao wote kwa pamoja watasaidia kuondoa tatizo la uhaba wa nishati hiyo muhimu ambayo inatajwa kuwa kichocheo kikuu cha ukuaji kiuchumi.
“Tunazunguka kukagua na kuangalia ni maeneo yapi yatatusaidia kuongeza kiasi cha uzalishaji umeme tunaouhitaji. Wazalishaji wadogo, wakubwa na wa kati wote watasaidia kufikia malengo yetu ya kuhakikisha tunakuwa na umeme mwingi na wa kutosha. Sote tunajua umeme ni ajira na umeme ni viwanda. Bila umeme hatuwezi kuwa na viwanda vya kutosha”,aliongeza Prof. Muhongo.
Katika hatua nyingine, Waziri Muhongo ameagiza TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kufanya majadiliano na TANWAT ambao pia ni wazalishaji wa nguzo za umeme , kufanya majadiliano na kampuni hiyo yenye uwezo wa kuzalisha nguzo 120,000 kwa mwaka, ili iuze nguzo hizo badala ya wakandarasi kuagiza nje ya nchi.
“REA na TANESCO watakuja hapa kuangalia nguzo hizi na kufanya ukaguzi kama zinakidhi viwango vya TANESCO. Ikiwa zinakidhi vigezo, REA wawaelekeze Wakandarasi kununua nguzo za TANWAT badala ya kununua nguzo nje kama ilivyo sasa ambapo wananunua nchi za Kenya, Uganda, Zambia na Afrika Kusini”, amesisitiza Prof. Muhongo.
Akikagua mradi wa Kufua umeme wa Maji (Mini Hydro) uliopo Uwemba nje kidogo ya mji wa Njombe, Prof. Muhongo ameagiza TANESCO kuandaa orodha ya vyanzo vya umeme vinavyotokana na maji na vilivyo katika gridi na visivyo katika gridi na kujadiliana na wazalishaji ili kukubaliana nao namna ya kuuziana umeme.
“Uzalishaji umeme kwa kutumia maji ndiyo rahisi zaidi.
TANESCO angalieni orodha hiyo na wao wawaeleze
Mikataba yao muone na mkubaliane namna ya kuuziana umeme. Bila umeme wa
mwingi na wa uhakika hatuwezi kuwa na viwanda vya kutosha,”ameongeza
Prof.
Waziri Muhongo ameongeza kuwa, ni wajibu wa Serikali kuwasaidia na kufanya kazi na wazalishaji wadogo wa umeme ili wasaidie kuongeza kiwango cha uzalishaji umeme na hivyo kuutaka uongozai wa Mkoa wa Njombe kufuatilia kwa pamoja na TANESCO suala hilo na kulifanyia kazi kwa karibu.
Waziri Muhongo ameongeza kuwa, ni wajibu wa Serikali kuwasaidia na kufanya kazi na wazalishaji wadogo wa umeme ili wasaidie kuongeza kiwango cha uzalishaji umeme na hivyo kuutaka uongozai wa Mkoa wa Njombe kufuatilia kwa pamoja na TANESCO suala hilo na kulifanyia kazi kwa karibu.
Aidha,
Prof.Muhongo amewaagiza TANESCO kuharakisha matengenezo ya mtambo
ulioharibika katika kituo cha kufua umeme cha Uwemba ili kuongeza
uzalishaji wa umeme wa uhakika.
Mbali na Mkoa wa Njombe katika ziara yake ya kutembelea miradi ya umeme, Prof Muhongo pia atatembelea Mikoa ya Ruvuma, Mbeya na iringa ambapo pia atakagua maeneo ya utafiti na uchimbaji wa Makaa ya Mawe.
Mbali na Mkoa wa Njombe katika ziara yake ya kutembelea miradi ya umeme, Prof Muhongo pia atatembelea Mikoa ya Ruvuma, Mbeya na iringa ambapo pia atakagua maeneo ya utafiti na uchimbaji wa Makaa ya Mawe.
No comments:
Post a Comment