Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, December 31, 2015

ZAIDI YA WAFANYAKAZI WA TANWAT 190 WASIMAMISHWA KAZI BAADA YA KIWANDA KIPYA CHA PLAY WOOD KUUNGUA USIKU WA KUAMIKIA JANA




SHUGHULI ZA UOKOAJI ZINAMALIZIKA NA SASA  WAFANYAKAZI WANAKWENDA KUENDELEA  NA MAJUKUMU YAO HUKU WENGINE WAKIAMBIWA WARUDI NYUMBANI HADI KIWANDA HICHO KITAKAPOPONA









MBUNGE WA JIMBO LA NJOMBE KUSINI EDWARD FRANZ MWALONGO AKIZUNGUMZA NA BAADHI YA MFANYAKAZI WA KIWANDA CHA TANWAT AKIWA KIWANDANI HAPO

 

 





AFISA UTAWALA WA KAMPUNI YA TANWAT EDMUND MUNUBI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSIANA NA HASARA NA  TUKIO ZIMA LA KUUNGUA KWA KIWANDA CHA TANWAT








GARI LA ZIMA MOTO NA UKOAJI MKOA WA NJOMBE LIKIWA ENEO LA TUKIO  KWAAJILI YA KUZIMISHA MOTO ULIOKUWEPO KWENYE KIWNADA HICHO





















HUKU WALIFANIKIWA KUZUIA MOTO USIFIKE  NA KUOKOA MALI ZA KIWANDA HICHO


HUKU NDIKO KULIKOOKOLEWA KUSIUNGUWE












MTANGAZAJI WA UPLANDS FM EMMANUEL SKAWA AKISALIMIANA NA MBUNGE WAKATI ANAWASILI KIWANDANI HAPO






MBUNGE WA JIMBO LA NJOMBE KUSINI EDWARD MWALONGO AKITEMBELEA ENEO LILILOUNGUA LA KIWANDA CHA TANWAT MJINI NJOMBE


















HUU NI MTAMBO ULIOSABABISHA KUTOKEA KWA MOTO HUO BAADA YA KUGONGA BOMBA LA MAFUTA UNAOITWA FOCAL LIFT KWA MUJIBU YA MAJIBU YA LUGHA YA KITAALAMU KIWANDANI HAPO






















RANGI ZA UKUTA ZILIZOWEKWA KWENYE BATI HIZO ZIMEKWAJUKA BAADA YA KUPATA JOTO LA MOTO MKUBWA NDANI YA KIWANDA







Kampuni Ya Tanwat Mjini Njombe Imelazimika Kuwasimamisha  Kazi Wafanyakazi  Mia 190 Waliokuwa Wakifanya Kazi Kwenye Kiwanda Cha Play Wood Kufuatia Kiwanda Hicho Kuteketea Kwa Moto  Na Kusababisha Hasara Ya Takribani Bilioni Moja Tukio Ambalo Limetokea  Majira Ya Saa Tisa  Usiku Wa jana.

Akizungumza Na Uplands Fm Afisa Utawala Wa Kampuni Ya Tanwat Edmund Munubi Amesema Hatua  Ya Kuwasimamisha Wafanyakazi Hao  Kwa Muda Usiyojulikana Imetokana Na Kuungua Moto Kiwanda Cha Play Wood  Ambapo Wakati Jitihada Za Kufanya Tathmini Ya Mali  Zilizoungua Wamelazimika Kuwasimamisha Kwa Muda  Hadi Kiwanda Hicho Kitakapo Tengenezwa.

Mnubi Amesema Kuungua Kwa Kiwanda Hicho  Katika Eneo La Boila Litokea  Baada Ya Dereva  Aliyekuwa Akiendesha Mashine Ya Kubebea  Mizigo Kurudisha Nyuma Mashine Hiyo Na Kugonga Bomba La Mafuta Na Kusababisha  Kutokea Kwa Moto Huo  Nakwamba Kwa Maelezo Ya Waliokuwepo Usiku Huo  Breki Zilikatika Kwenye Mashine  Na Kutokea Tukio Hilo.

Kwa Upande Wake Wafanyakazi  Wa Kiwanda Hicho Wameelezea Masikitiko Yao Baada Ya Kuungua Kwa Kiwanda Hicho Na Kuuomba Utawala Wa Kampuni Hiyo Kuwatafutia Nafasi Nyingine Ya Kazi Wakati Wakisubiria  Hatima Ya Kiwanda Kilichoungua Ili Waweze Kuendesha Maisha Yao Na Familia Zao.

Mbunge Wa Jimbo La Njombe Kusini Edward Franz Mwalongo Akiwa Kwenye Kiwanda Hicho Ametoa Pole Kwa  Wamiliki Wa Kiwanda Hicho Na Wafanyakazi Kutokana Na Uzalishaji Kusimama  Na  Kupongeza Jeshi La Zima Moto Na Uokoaji Kwa Jitihada Walizofanya   Huku Msemaji Wa Jeshi La Zima Moto Na Uokoaji  Akiomba Ushirikiano Kuoneshwa Pindi Matukio Kama Hayo Yanapotokea.

No comments:

Post a Comment