Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, December 26, 2015

SAKATA LA MADINI AINA YA MAWE KATIKA MTAA WA SIDO BADO LINAENDELEA KUTAFUTIWA UFUMBUZI YA NANI AMILIKI LESENI SERIKALI YA MTAA AMA KIKUNDI CHA WACHIMBAJI CHA JUA KALI


TATIZO NI NANI AMILIKI LESENI YA ENEO  SERIKALI YA MTAA NDIYE MWENYE ENEO  ANATAKIWA KUMILIKI LESENI  KIKUNDI CHA JUA KALI NACHO KINATAKA KUMILIKI LESENI  SASA NANI MWENYE HAKI YA KUMILIKI LESENI  WANANCHI KWENYE MKUTANO WA HADHARA WAADHIMIA  KAMA HAWATAKI WAONDOLEWE WOTE WACHIMBAJI UTARATIBU WA KUWASAJIRI UANZE UPYA ENEO LA SERIKALI YA MTAA WA SIDO.

 HAWA NI WACHIMBAJI WA MADINI WADOGOWADOGO WAKIWA KWENYE MKUTANO

 MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA WA SIDO RICHARD BIMBIGA AKIWA NA  AFISA MADINI JOHN MAGANGA WALIPOTEMBELEA KWA MARA YA KWANZA ENEO LA MACHIMBO .






 MADINI AINA YA MAWE  YANAYOPATIKANA ENEO LA MTAA WA SIDO
 KOKOTO  ZINAZOANDALIWA NA WACHIMBAJI HAO WADOGO NJOMBE

Serikali Ya Mtaa Wa Sido Mjini Njombe Imesema Bado Inaendelea Na Jitihada Za Kuhakikisha Inakwenda Kukata Leseni Ya Machimbo Ya Madini Ya Mawe Yaliopo Eneo La Ganga Lyandefu  Ambalo  Wachimbaji Waliopo Wanataka Kukata Reseni Ya Umiliki Wake   Huku Serikali Ya Mtaa Huo Ikisema  Anayestahili Kumiliki Reseni Ni Mtaa Wa Sido Na Siyo  Kikundi.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Mwenyekiti Wa Serikali Ya Mtaa Wa Sido Richard Bimbiga  Kufuatia Makubaliano Ya Wananchi Wa Mtaa Huo  Ya Kwenye Mkutano Wa Hadhara Uliofanyika  Decemba 20 Mwaka Huu Ambao Makubaliano Ya Wananchi  Wake Ni Kutaka Eneo Hilo La Machimbo  Reseni Yake Imilikiwa Na Serikali Ya Mtaa Ili  Kila  Mmoja Anufaike  Na Machimbo Hayo.
CUE....MWKT  SIDO
Aidha  Bimbiga  Amesema Mmili Wa Eneo Hilo La Machimbo Ni Serikali Ya Mtaa  Wa Sido Na Kwamba Kutokana Na Wananchi Kutaka Serikali Imiliki  Leseni Ya Machimbo Hayo ,Wachimbaji Waliopo Sehemu Hiyo  Kwa Sasa Wanapaswa Kufuata Utaratibu Wa Serikali Ya Mtaa   Tofauti Na Hapo  Hatua Za Kuwaondoa Kinguvu Zitafuata Na Usajiri Wa Wachimbaji  Utaanza Upya.

 Afisa Mtendaji Wa Serikali Ya Mtaa Wa Sido Rehema Ngairo Amesema Hapo Awali Kabla Ya Kuupata Uongozi  Uliotokana Na Uchaguzi Wa Mwezi Decemba Mwaka Jana Walikuwa Wakichukua Ushuru  Kwenye Eneo Hilo Lakini  Watu Wa Madini Walipoingia Na Kushawishi Wachimbaji Hao Wawe Na Leseni  Ndipo Serikali Ya Mtaa Huo Iliamua Kuacha Kuchukua Ushuru  Kutokana Na Muingiliano Uliokuwepo.

Awali Wakizungumza Kwa Nyakati Tofauti Baadhi Ya Wananchi Wa Mtaa Wa Sido Wamesema Kutokana Na Makubaliano Waliokubaliana Kwenye Mkutano Wa Mtaa Huo Ni Vema Serikali Ya Mtaa Ikate Leseni Ya Machimbo Hayo  Ili Mtaa Mzima Unufaike Na Eneo Hilo  Huku Wakitaka Wachimbaji Kuacha Kung'ang'ania Kukata Leseni Hiyo Kwani Mmiliki Wakr Ni Serikali Ya Eneo Hilo.

Hivi Karibuni Maafisa Madini Mkoa Wa Njombe Waliagiza Wachimbaji  Hao Kukubaliana Na Serikali Ya Mtaa  Ili Kufikia Maamuzi  Ya Umiliki Wa Leseni  Na Endapo Hawatafikia Mwafakata Wa Sakata Hilo  Watalazimika Kufungia Eneo Hilo Lisitumiwe Na Wachimbaji  Wowote  Lakini Wachimbaji  Hao Bado Hawajaridhika Na Maamuzi Hayo.

No comments:

Post a Comment