Wakazi wa
Kahe wakifatilia tamasha la Halo Xmas katika Wilaya ya Kahe
Msanii Msami akiburudisha wanakijiji wa Kahe katika
tamasha la Halo Xmas
Msanii
Shilole akiimba wakati wa tamasha la Halo Xmas lililofanyika wilaya ya
Kahe.
Wakazi wa
Ruangwa wakifuatilia burudani ya tamasha la Halo Xmas lililofanyika katika
uwanja shule ya msingi Likangala.
Matamasha ya Halotel yafunika nchi
nzima
Matamasha
ya Halo Xmass yaliyoandaliwa na kampuni ya Halotel katika mikoa mitano nchini
yamefunika kwa kutoa burudani nzuri na kupata mahudhurio makubwa ya mashabiki.
Matamasha
hayo ambayo yamefanyika wilaya za Tukuyu, Ruangwa, Moshi Vijijini, Chato pamoja
na Mpwapwa, yamejumuisha wasanii wa bongo fleva pamoja na burudani nyingine
kutoka kwa wasanii wa maeneo hayo.
Tamasha
la Halo Christmass wilayani Tukuyu limefanyika katika uwanja wa Tandale na
burudani imetolewa na wasanii Tundaman na Makomando.
Kwa
upande wa Ruangwa, tamasha limefanyika katika viwanja vya shule ya msingi
Likangala, na kutumbuizwa na wasanii Amini pamoja na Matonya, wakati Mpwapwa tamasha
limefanyika katika viwanja vya Mgambo likitumbuizwa na wasanii Madee na
Malaika.
Wakazi
wa Chato pia wamepata burudani ya kufunga mwaka katika viwanja vya Stand ya
Zamani kutoka kwa msanii Shetta na Baraka Da Prince.
Moshi
vijijini pia wamefurahia tamasha la Christmass kwa burudani kutoka kwa Shilole
na Msami zilzofanyika katika viwanja vya Kaye.
Baadhi
ya mashabiki waliohudhuria tamasha hilo Moshi wameipongeza Halotel kwa
kuwaandalia tamasha hilo wakisema hii ni mara ya kwanza burudani kubwa imefika
kijijini kwao.
‘Makampuni
mengi hupenda kufanya matamasha ya aina hii mijini, lakini kwa Halotel ni
tofauti, kama namna huduma zao zilivyo za kipekee’ alisema Bi Halima Sanare,
mkazi wa kijiji cha Kaye.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Halotel bwana Nguyen Thanh Quang, amesema matamasha hayo ya Halotel yalilenga
kuwaleta watumiaji wa Halotel pamoja na kuwapa burudani ya kufunga mwaka.
‘Hii ni zawadi kwa watumiaji wa mtandao wetu na wateja wapya wanaotaka
kujiunga na familia yetu ya Halotel, na ndio maana tunawafata katika maeneo yao
yalipo’ alisema Quang.
Quang pia amewaahidi wateja wa Halotel kuwa mtandao wake unatarajia
kuleta mabadiliko katika sekta ya mawasiliano nchini kwa kuwapa wateja wake
zaidi ya huduma za simu.
Msanii
Sheta akiimba na mtoto katika tamasha la Halo Xmas lililofanyika uwanja wa
stendi ya zamani Chato.
Madee
akiburudisha mashabiki wa Mpwapwa katika uwanja wa Mgambo
Msanii
Matonya akiimba katika uwanja wa Ruangwa wakati wa tamasha la Halo Xmas.
Baraka Da
Prince akiimba wakati wa tamasha la Halo Xmas mjini Chato
No comments:
Post a Comment