Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, February 21, 2015

WAFANYABIASHARA WA SOKO LA MBAO WAANDAMANA HADI OFISI YA MKURUGENZI KUSHINIKIZA WATENGENEZEWE BARABARA YA SHIPO -KAMPALAGE

Wafanyabiashara Wa Soko La Mbao Na Wamiliki Wa Magari  Mbalimbali  Yanayoelekea Mtaa  Wa Kambalage Leo Wameandamana Hadi  Ofisi Ya Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Ili Kushinikiza  Uwezekano Wa Kutengeneza Barabara Hiyo Ambayo Imeshindwa Kupitisha Magari Ya Mizigo Na Abiria.

Wakiongea  Na Uplands Fm Wafanyabiashara  Na Wamiliki  Wa Magari Hayo Wamesema Kuwa  Wameshindwa Kusafirisha Mizigo Yao Ya Mbao Na Mali Nyingine Kwa Muda Wa Siku Tatu Kutokana Na Kuharibika Kwa Barabara Hiyo  Ambapo  Wameomba Serikali Iharakishe Kuwarekebishia Miundombinu Hiyo  Ili Kufanikisha Kusafirisha Bidhaa Zao.

Aidha Wafanyabiashara Hao Wamesema   Kutokana Na Kushindwa Kusafirisha  Mizigo Yao  Huenda Wakashindwa Kurejesha Mikopo Waliochukua Kwenye Taasisi Za Kifedha   Huku Wakisema Wanashindwa Kuelewa  Kwanini Serikali Inashindwa Kuboresha Miundombinu Hiyo Ikiwa Ushuru Wanalipa  Shilingi Laki Tatu Kwa Kila Mfanyabiashara.

Wafanyabiashara Hao Walipofika Kwa Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Wamefanikiwa Kupewa Ushirikiano  Ambapo Mkurugenzi Na Muhandis Wamefika Eneo La Tukio Na Kupeleka Mafuta Ya Gari Hilo La Barabara Ambalo Baada Ya Dakika Chache  Liliharibika  Na Kisha Wafanyabiashara WaKaamua Kufunga Barabara Ili Mgari Yasipite.

Katibu Wa Wafanyabiashara Wa Mbao  Mkoa Wa Njombe Gipson Nyondo Amesema Kuwa Licha Ya Jitihada Za Kwenda Kwa Mkurugenzi Kuomba  Mafuta Yapelekwe Kwenye Gari La Kulimia Barabara  Hiyo Ambalo Limepakiwa Kwenye Eneo Hilo Korofi Tangu Jana Asubuhi Hakuna Mafanikio Walioyapata Baada Ya Gari Hilo Kuharibiuka.

Bwana  Nyondo Amesema Kuwa Walipo Kwenda Kwa Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji Walipelekewa Mafuta Rita Sitini Za Kujaza Kwenye Gari  Hilo Ili Kurekebisha Eneo Hilo  Bila Mafanikiwa Kutokana Na Kuharibika Kwake Ambapo Amesema Tatizo La Miundombinu Hiyo Limetoka Likiwasumbua Kwa Takribani Miezi Minne Sasa.

Mwenyekiti Wa Mtaa Wa Kambalange Bwana  Braison Mgaya  Amesema Amekuwa Akifika Katika Ofisi Ya Mkurugenzi  Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Kueleza Changamoto Zinazowakabili  Lakini Hakuna Utekelezaji Wowote Kuhusiana Na Kutengeneza Miundo Mbinu Hiyo.

Kwa Upande Wake Kaimu Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Akizungumza Akiwa Eneo La Tukio Ambapo Barabara  Inatakiwa Kurekebishwa  Venance Msungu Akiwa Na Mhandis Wa Ujenzi Ibrahim Mkangara Wamesema Wanakwenda Kufuata Gari Lingine La Kwenda Kurekebisha Eneo Hilo Baada Ya Kuona Gari Lililokuwa Likitegemewa Kuharibika.

 Bwana Msungu Amewasihi Wafanyabiashara Hao Kuwa Na Subira Wakati Halmashauri Ikilishughulikia Tatizo Hilo Mara Moja  Ambapo Hadi Tunaingia Mitamboni Gari Hilo Lilikuwa Bado Halijafika Eneo La Tukio Ili Kurekebisha  Barabara Hiyo Na Magari Yaweze Kupita.


No comments:

Post a Comment