Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, October 11, 2014


ZIARA YA KATIBU MKUU WA CMCM,NDUGU KINANA - JIMBO LA MUFINDI KUSINI

 Vitalu vya miche ya miti vinavyomilikiwa na Umoja wa Vikundi vya Kijamii wilaya ya Mufindi (UVIKIMU)
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kumwagia maji vitalu vya miche ya miti vinavyomilikiwa na Umoja wa Vikundi vya Kijamii wilaya ya Mufindi (UVIKIMU)
 Shamba la chai Ngwazi
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuchuma chai pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye shamba la chai Ngwazi wilaya ya Mufindi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akichuma chai, ambapo alitaka wakulima wadogo pia wasaidiwe ili kufanikisha kilimo ch chai kwani chai ikisimamiwa vizuri itasaidia  kuinua uchumi wa nchi na kumpatia mkulima kipato kizuri.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia),Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu (katikati) na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwapungia mkono wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya mkutano Nyololo njia panda.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Jimbo la Mufindi Kusini ambapo aliwaambia anawapongeza wapinzani kwa kukubali Katiba iliyopendekezwa na amesema kama walivyotangaza kuwa watashawishi wapiga kura wasiipigie basi na CCM itawashawishi wapiga kura waipigie .
 Mwenyekiti wa CCM Ndugu Jesca Msambatavangu akihutubia wananchi kwenye kiwanja cha mkutano Nyololo njia panda
 Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini Mendrad Kigola akiwahutubia wananchi wake wa kata ya Nyololo ambapo alisema maji bado hayajapatiwa ufumbuzi zinahitajika zaidi ya milioni 800 kutatua tatizo la maji.
 Hii gari ya aina yake ilikuwa kivutio kwenye mkutano.
 Wananchi wakisikiliza mkutano wakiwa juu ya uzio wa kiwanja cha Nyololo njia panda
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa pamoja na mtoto Meliko Mpevu,na Afisa wa Chama Makao Makuu Edward Mpogolo(watatu kutoka kulia) na wadau wengine wa CCM wilaya ya Mufindi wakifuatilia kwa makini mkutano unavyoendelea.
 Wananchi wakisikiliza kwa makini
 Wananchi wakishangilia hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa jimbo la Mufindi Kusini ambapo aliwaambia tabia ya kufanya kazi kwa mazoea kwa watumishi wengi wa serikali kumechangia sana kushusha nidhamu na kutofanya kazi kwa ufanisi ,Katibu Mkuu pia alisema kuwekwe utaratibu mzuri utakaopunguza malalamiko kwenye utoaji wa vibali vya kuvuna mbao,pia aliwaambia wananchi wa Mufindi kuwa vijiji 46 vitapata umeme ikiwa vijiji 35 vitapata kupitia mradi wa Umeme Vijijini (REA) na 11 vitapata kupitia mradi wa Mwenga Hydro.
 Josephat Sebadi Soda aliyekuwa Katibu wa Chadema kata ya Igowole akitangaza rasmi kurudi CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mikutano Nyololo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambapo yeye pamoja na wenzake 27 wamerudi na kujiunga na CCM
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea kadi na bendera za Chadem kutoka kwa aliyekuwa Katibu wa Chadema kata ya Igowole  Josephat Sebadi Soda aliyeamua kujiunga na CCM.
 Zaidi ya wanachama wapya 485 wamejiunga na CCM wilaya ya Mufindi.
 Wanachama wapya wakila kiapo.
 Mzee alishindwa kuvumilia na kuamua kuyarudi
 Wasanii wa CCm Band Mufindi wakitoa burudani baada ya mkutano kumalizika.
 Wananchi wakiserebuka pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kumaliza mkutano .
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (katikati)na Katibu wa CCM wilaya ya Mufindi Miraji Mtaturu  (kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wasanii wa bendi  ya CCM Band Mufindi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiangalia kasha la albamu ya bendi ya CCM Mufindi ambayo walizindua albamu inayokwenda kwa jina la ILANI.

No comments:

Post a Comment