Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, July 11, 2014

MKUTANO MKUU WA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA NJOMBE LA HITIMISHWA JANA









 MHANDIS WA UJENZI WILAYA YA NJOMBE



 MKURUGENZI HALMSHAURI YA WILAYA YA NJOMBE PAUL MALALA AKIJIBU MASWALI YA WAJUMBE WA BARAZA HILO


Mkutano mkuu wa baraza la madiwani umetaka wawekezaji mbalimbali Wilayani Njombe kusaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili jamii inayowazunguka  ikiwemo miundombinu ya barabara,zahanati na huduma nyingine kama ahadi za wawekezaji  walizotoa wakati wa kusajiliwa.

Kauli hiyo imetolewa na wajumbe wa mkutano mkuu wa baraza la madiwani wilaya ya Njombe kufuatia kuwepo kwa baadhi ya wawekezaji kushindwa kutekeleza ahadi zake  ambazo huahidiwa wakati wanakaribishwa kuwekeza eneo husika ambapo wametolea mfano wananchi wa vijiji vya Lupembe kushindwa kusafirisha mazao  mbalimbali ikiwemo chai na mazao mengine ikiwa wawekezaji wa kiwanda cha chai Ikanga wapo wanasubiri serikali itengeneze.

Miongoni mwa wawekezaji waliolalamikiwa kushindwa kutekeleza ahadi zake za kuboresha huduma kwa wananchi  ni pamoja na kampuni ya kiwanda cha Ikanga ambao waliahidi kujenga mawodi ya kituo cha afya Lupembe,Zahanati ya Kijiji cha Wangingyi  na kutengeneza miundombinu ya barabara katika maeneo ya wananchi yanayozunguka  maeneo ya uwekezaji lakini hadi sasa wamiliki wa kiwanda hicho hawajafanya hivyo.

Akijibu maswali ya wajumbe wa baraza hilo mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe Paul Malala amesema kuwa halmashauri inatarajia kumuita muwekezaji wa kiwanda cha chai Ikanga kwenye balaza la madiwani  litakalo fanyika mwezi augost mwaka huu   ili wajumbe waweze kujua uwepo wa kampuni hiyo huku mhandis wa ujenzi wa halmashauri hiyo akisema serikali pia itaingiza kwenye bajeti  ya mwaka 2014/2015 na kuweka fedha ya dharula.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Valence Kabelege  akifunga mkutano huo amesema kuwa  maazimio yote yaliazimiwa na wajumbe wa mkutano huo yanatakiwa kutekelezwa huku akisema kuwa  kila mjumbe ameonekana kulalamikia fedha iliyotolewa kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya kila kata kwamba hazikidhi malengo yaliokusudiwa na kwamba hali hiyo inatokana  na udhaifu wa ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Amesema kuwa kulingana na bajeti iliyokuwepo kuwa ndogo  imesababisha kila kata kupata fedha isiyokidhi matakwa ya miradi iliyoibuliwa ambapo amesisitiza kuwepo kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani  ambayo yataisaidia halmashauri kujiendesha yenyewe.


No comments:

Post a Comment