KWAYA YA MT.JOSEPH IKIWA KWENYE WODI LA AKINA MAMA WALIOJIFUNGUA
MWENYEKITI WA KWAYA YA MT.JOSEPH BWANA MARIO LUGENGE AKIZUNGUMZA KABLA YA KUKABIDHI MSAADA HUO.
MLEZI WA KWAYA HIYO BWANA EDWARD FRANCIS MWALONGO AKIZUNGUMZA WAKATI WA KUKABIDHI MSAADA HUO.
MAKABIDHIANO HAPA YANAENDELEA KUFANYIKA
MGENI RASMI AKIMFUNIKA MAMA NA MTOTO WAKE AMBAE AMETOKA KUJIFUNGUA
KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE BWANA HAMISI H. CHINDUL AKIZUNGUMZA BAADA YA KUPOKEA MSAADA HUO
kwaya ya St.Joseph hapa inaimba wimbo wa shukrani wakiwa katika wodi la akina mama waliotoka kujifungua kibena
HUYU NI MGANGA MKUU WA HOSPITALI HIYO DR.JAMES LIGWA
Siku chache baada ya shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii mkoa wa Njombe NSSF
Kukabidhi msaada wa taa mbili kwaajili ya chumba cha upasuaji katika hospitali ya Kibena
wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 11,kwa mara nyingine tena Mkuu wa mkoa wa
Njombe Keptain Mstaafu Aseri Msangi amepokea msaada wa mashuka na mablanketi sabi
wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili.
Akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo mwenyekiti wa kwaya ya St.Joseph ya
kanisa Katholiki Jimbo la Njombe bwana Mario Lugenge amesema kuwa msaada huo ni
mwendelezo wa kanisa Katholiki kupitia kwaya mbalimbali za kanisa hilo kukabidhi
misaada kwa watu wasiyojiweza,yatima na wagonjwa kama maandiko ya biblia
yanavyosema.
Aidha bwana Lugenge amesema kuwa kufanikisha zoezi hilo kumetokana na mapato ya
mkanda a Vedeo ambao walitengeneza pamoja na kupata michango kutoka kwa wadau
mbalimbali wa mkoa wa Njombe ambao waliichangia kwaya hiyo na kufanikisha kununua
mashuka 35 na mablanketi 35 ambayo ni mazito kulingana na baridi ya msimu huu.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Njombe Keptain Mstaafu Aseri Msangi
mara baada ya kupokea msaada huyo ,Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Njombe bwana
Hamisi Chindul ameshukuru kwa hatua hiyo na kuwaomba wanakwaya hao kuendelea na
moyo wa kuwasaidia wasiyojiweza huku taasisi nyingine zikipaswa kuiga mfano huo
kuwasaidia wagonjwa na vifaa vya hospitali hiyo.
Bwana Chindul amewataka wauguzi wa hospitali hiyo kuvitunza vifaa mbalimbali
ambavyo vimekuwa vikitolewa na watu wenye mapenzi mema kama msaada kwa
wagonjwa na marekebisho ya hospitali ili mashirika na watu wenye moyo wa kusaidia
hospitali hiyo wasikatishwe tamaa na utunzaji na matumizi ya vifaa hivyo.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Hospitali ya Kibena Dr James Ligwa akizungumza
kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Njombe amepongeza kwa hatua hiyo
ya kwaya ya St. Joseph kukabidhi msaada huo na kwamba atahakikisha vifaa hivyo
vinatumika kwa malengo yaliokusudiwa na kuvitunza visiharibike.
Hospitali ya mkoa wa Njombe ya Kibena imekuwa ikijipatia misaada mbalimbali kutoka
kwa mashirika,taasisi na watu binafsi tangu ilipokabidhiwa kuwa ya mkoa ambapo siku
chache zilizopita shirika la Hifadhi ya Jamii mkoa wa Njombe NSSF na makanisa mjini
Njombe yameanza kupeleka misaada hiyo ili kuboresha mazingira yake na kuwasaidia
wagonjwa baadhi ya huduma.
Kukabidhi msaada wa taa mbili kwaajili ya chumba cha upasuaji katika hospitali ya Kibena
wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 11,kwa mara nyingine tena Mkuu wa mkoa wa
Njombe Keptain Mstaafu Aseri Msangi amepokea msaada wa mashuka na mablanketi sabi
wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili.
Akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo mwenyekiti wa kwaya ya St.Joseph ya
kanisa Katholiki Jimbo la Njombe bwana Mario Lugenge amesema kuwa msaada huo ni
mwendelezo wa kanisa Katholiki kupitia kwaya mbalimbali za kanisa hilo kukabidhi
misaada kwa watu wasiyojiweza,yatima na wagonjwa kama maandiko ya biblia
yanavyosema.
Aidha bwana Lugenge amesema kuwa kufanikisha zoezi hilo kumetokana na mapato ya
mkanda a Vedeo ambao walitengeneza pamoja na kupata michango kutoka kwa wadau
mbalimbali wa mkoa wa Njombe ambao waliichangia kwaya hiyo na kufanikisha kununua
mashuka 35 na mablanketi 35 ambayo ni mazito kulingana na baridi ya msimu huu.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Njombe Keptain Mstaafu Aseri Msangi
mara baada ya kupokea msaada huyo ,Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Njombe bwana
Hamisi Chindul ameshukuru kwa hatua hiyo na kuwaomba wanakwaya hao kuendelea na
moyo wa kuwasaidia wasiyojiweza huku taasisi nyingine zikipaswa kuiga mfano huo
kuwasaidia wagonjwa na vifaa vya hospitali hiyo.
Bwana Chindul amewataka wauguzi wa hospitali hiyo kuvitunza vifaa mbalimbali
ambavyo vimekuwa vikitolewa na watu wenye mapenzi mema kama msaada kwa
wagonjwa na marekebisho ya hospitali ili mashirika na watu wenye moyo wa kusaidia
hospitali hiyo wasikatishwe tamaa na utunzaji na matumizi ya vifaa hivyo.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Hospitali ya Kibena Dr James Ligwa akizungumza
kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Njombe amepongeza kwa hatua hiyo
ya kwaya ya St. Joseph kukabidhi msaada huo na kwamba atahakikisha vifaa hivyo
vinatumika kwa malengo yaliokusudiwa na kuvitunza visiharibike.
Hospitali ya mkoa wa Njombe ya Kibena imekuwa ikijipatia misaada mbalimbali kutoka
kwa mashirika,taasisi na watu binafsi tangu ilipokabidhiwa kuwa ya mkoa ambapo siku
chache zilizopita shirika la Hifadhi ya Jamii mkoa wa Njombe NSSF na makanisa mjini
Njombe yameanza kupeleka misaada hiyo ili kuboresha mazingira yake na kuwasaidia
wagonjwa baadhi ya huduma.
No comments:
Post a Comment