Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, January 29, 2014

WATU SITA WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUVUNJA NA KUIBA NA KUJERUHI KWA NJIA YA LUNGU NA NONDO NA KUIBA MALI MBALIMBALI NJOMBE


KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE SACP FULGENCE NGONYANI AKIWA OFISINI KWAKE LEO.
Jeshi la polisi mkoa wa Njombe linawashikiliwa watu sita kwa tuhuma za kuhusika na kuvunja

store iliyoko mtaa wa masasi na kuiba mali mbalimbali za mfanyabiashara Merick Vintan Mgina

mkazi wa mtaa wa Mgendela  kata ya Njombe mjini zenye thamani ya shilingi milioni nane mali ya

Merick Vintan Mgina pamoja na tukio la pili la wizi wa shilingi milioni sita na elfu themanini mali ya Benki ya NBC ya Njombe mjini.

Akizungumza na mtandao huu www.michaelngilangwa.blogspot.com kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe SACP Fulgence

Ngonyani amesema kuwa kufuatia tukio hilo jeshi la polisi liliendesha msako mkali na kufanikiwa

kuwakamata watuhumiwa watano Joseph Sanga mkazi wa kibena,Wito James Mlowe mkazi wa

mwenmbetogwa mkoani Iringa,Rajabu Makweta,Michael Kilumile na Geoge Kilumile wakazi wa

mjini Njombe.

Aidha kamanda Ngonyani amesema katika msako uliofanyika januari 27 mwaka huu watuhumiwa

Geoge Kilumile na Michael Kilumile walikamatwa wakiwa na mali za wizi walizoiba mnamo

januari 26 mwaka huu majira ya saa saba usiku katika mtaa wa masasi kwenye store ya

mfanyabiashara Merick Vintan Mgina ambazo ni konyagi box 11,red bull katoni 10 huku mali

nyingine zikiendelea kutafutwa.

Kamanda Ngonyani amesema kuwa katika msako huo pia walifanikiwa kumkamata mkazi mmoja

wa mtaa wa Matalawe Jackson Simkoko baada ya kukutwa na fedha zilizoibiwa katika ghala la

mbolea la kampuni ya Primium lililoko maeneo ya Banki ya NBC  mjini Njombe .

Katika tukio  lingine kamanda Ngonyani amesema  watu wawili Hezron Fate na Stela Lugona

wamejeruhiwa na kuporwa mali mbalimbali na fedha shilingi milini moja  na laki tatu na watu

wasiyofahamika baada ya kuvunja nyumba yao    ambapo jumla ya thamani ya vitu na fedha ni

shilingi milioni mbili na laki mbili  ziliporwa na watu hao na kuwajeruhi kwa kutumia lungu na

nondo na kwamba hakuna mtuhumiwa anaeshikiliwa na jeshi hilo.

Amesema kuwa tukio lingine mkazi mmoja wa kijiji cha Itipingi kata ya Mahongole Albano

Kilumile 16 alifariki dunia baada ya kupigwa na radi kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na

upepo iliyonyesha  mnamo january 27  na kusababisha kifo hicho.



No comments:

Post a Comment