Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, December 12, 2016

SHEKHE WA WILAYA YA NJOMBE MICDAD DINGADINGA AKEMEA NJAMA ZA KIKUNDI KINACHOTAKA KUVURUGA AMANI MSIKITINI


 
 SHEKHE WA WILAYA YA NJOMBE MICDAD DINGADINGA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSIANA NA KUAHIRISHWA KWA SHEREHE YA MAURIDI KWA NJOMBE NA KUHUSIANA NA KIKUNDI KINACHOTAKA KUVURUGA AMANI NA UTULIVU KWENYE MSIKITI HUO
 MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI KATIKA MSIKITI MKUU WA NJOMBE MJINI JUMA LUKUVI

 JUMA LUKUVI MWENYEKI WA ULINZI MSIKITI MKUU WA NJOMBE MJINI




NJOMBE

Wakati waumini wa dini ya kiislamu wakiadhimisha sherehe ya kuzaliwa kwa Mtume Muhamed Nchini Kote,Waumini wa dini hiyo   wameingiwa na hofu ya kutokea kwa uvunjifu  wa amani katika msikiti Mkuu wa Njombe Mjini  kutokana na kudaiwa kuwepo kwa kundi la watu wanaotaka kuharibu amani iliyopo msikitini hapo.

Kauli hiyo imetolewa na Shekhe Wa Wilaya Micdadi Dingadinga  wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake Kuhusiana na  Njombe kuahirisha  sherehe ya kuzaliwa kwa mtume Muhamad  ambayo waumini wa  Wilaya ya Njombe wataadhimisha Decemba 24 mwaka huu na kusema kuwa kumeibuka kikundi kinachotaka kuharibu amani ya waumini wa msikiti huo.

Shekhe Dingadinga  amesema viongozi wa msikiti Mkuu wa Njombe Mjini tayari  wamejiandaa kukabiliana na tatizo lililopo kwenye msikiti huo kwani wametoa taarifa kwa vyombo vya dola  kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya Msikiti Mkuu wa Njombe Mjini  ili kuimarisha amani ya waumini wa dini hiyo.

Kuhusu sherehe ya Maurid  Shekhe Dingadinga amesema waumini wa dini  hiyo  wanaadhimisha sherehe hiyo kwaajili ya kukumbuka historia ya kuzaliwa kwa Mtume Muhamad  ambaye katika itikadi za uislamu ni mtume wa mwanzo pia ni mtume wa mwisho ambaye amezaliwa siku ya jumapili kuamkia jumatatu katika Nchi ya Maka aliyeizungumza kwa ufasaha zaidi dini ya kiislamu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ulinzi  wa Msikiti mkuu wa Njombe Mjini Musa Lukuvi amewatoa hofu waumini wa dini ya Kiislamu katika msikiti huo kwamba  kikundi kinachotaka kuvuruga amani kitakwenda kuchukuliwa hatua za kisheria pindi kitakapojaribu kufanya tukio la uharifu  ambapo usalama umeimarishwa kwa kushirikiana na  jeshi la polisi.

Sherehe Ya Maurid Kitaifa hapo jana imefanyika katika Mkoa wa Singida Mgeni rasmi akiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasimu Majaliwa ambapo kwa Wilaya ya Njombe imeahirishwa hadi tarehe 24 mwezi huu itakapoadhimishwa kwani sherehe hiyo inakwenda hadi decemba 29 kwaajili ya waumini wa dini hiyo kukumbuka Historia ya kuzaliwa kwa Mtume Muhamad .


No comments:

Post a Comment