Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 4, 2016

WANANCHI IDINDILIMUNYO KATA YA IGWACHANYA WANGING'OMBE WAANDAMANA KUSHINIKIZA ASIHAMISHWE MWALIMU WA SHULE YA MSINGI ILIYOPO KIJIJINI HAPO


 HAWA NI WANANCHI WA KIJIJI CHA IDINDILIMUNYO WILAYANI WANGING'OMBE MKOANI NJOMBE WAKIWA KWENYE MAANDAMANO YA KUELEKEA KWA MKURUGENZI  WA WILAYA HIYO.
 DIWANI WA KATA YA IGWACHANYA ANTONY MAHWATA AKIWA KWENYE KIKAO CHA DHARULA CHA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA  WA WILAYA YA WANGING'OMBE  AKIWA NA KWENYE MAWAZO JUU YA KUANDAMANA KWA WANANCHI HAO KWENYE KATA YAKE.
 AFISA ELIMU SHULE ZA MSINGI WILAYA YA WANGING'OMBE  MWALIMU  HARUNA SEREMANI AKITOA TAARIFA YA SHULE ZENYE WALIMU WACHACHE ZAIDI KULIKO SHULE HIYO KWAMBA KUNA SHULE  WILAYA YA WANGING'OMBE ZINAWALIMU WATATU.
 HUYU NI MWENYEKITI WA KIJIJI CHA IDINDILIMUNYO GODEN KASANGA AKIZUNGUMZA JUU YA KILE KILICHOWAPELEKA KWA MKURUGENZI WA WILAYA HIYO.

 MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE  ALLY KASINGE AMBAYE NI MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA HIYO.

 MKURUGENZI WILAYA YA WANGING'OMBE  AMINA KIWANUKA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA IDINDILIMUNYO BAADA YA KUWASILI KWENYE UKUMBI WA KIKAO HICHO CHA DHARULA.



 HAPA WANANCHI WANATOKA KUELEKEA MAKWAO BAADA YA KUPOKEA USHAURI KUTOKA KWA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA

 HAPA NI SAFARI BILA MAANDAMANO INAANZA  YA KUELEKEA NYUMBANI KWAO IDINDILIMUNYO


Wananchi Wa Kijiji Cha Idindilimunyo  Kata Ya Igwachanya Wilayani Wanging'ombe  Leo  Wamefanya Maandamano Ya Amani  Yasiyo  Zingatia Taratibu Za Kisheria  Hadi Kwa Mkurugenzi  Ili Kushinikiza  Halmashauri Hiyo  Isimuhamishe Mwalimu Wa Shule Ya  Msingi Idindilimunyo  Kwenda Shule Ya Msingi Lyamluki  Kwa Kile Walichodai Kuwepo Kwa Upungufu  Wa Walimu.

Wakizungumza Na Uplands Fm  Baadhi Ya Wananchi Wa Kijiji Cha Idindilimunyo Wilayani Wanging'ombe  Wamesema  Wanashindwa Kufahamu Sababu Ya Mkurugenzi Wa Halmashauri Hiyo Kumuhamisha Mwalimu Huyo  Pasipo Kuwapelekea Mwalimu Mwingine  Wa Kuziba Nafasi Ya Anayehama  Ikiwa Bado Wanauhitaji Wa Walimu Watatu Kuziba Myanya Ya Walimu  Waliostaafu Mwakajana. 

Aidha  Wananchi Hao Wakiongozana Na Mwenyekiti  Goden Kasanga Wamelaumu Uongozi Wa Kata Ya Igwachanya Kuwa Huenda Umefanya  Njama  Za Kumuhamisha Mwalimu Huyo  Kupitia  Mwenyekiti Wa Halmashauri Ambaye  Ni Diwani Wa Kata  Hiyo Kutokana Na  Wananchi Hao Kugomea Kuchangia  Fedha Za Madawati  Kwa Kile Walichodai  Wanajenga Vyoo Kwanza Ndipo Madawati Yafuate Mwakani.

Akizungumza  Kwenye Kikao Cha Dharula Mwenyekiti Wa Kamati Ya Ulinzi Na Usalaama  Ambaye  Ni Mkuu Wa Wilaya Ya Wanging'ombe Muhamed Ally Kasinge  Amewaonya Wananchi Hao Kwamba  Wamekiuka  Kanuni Na Sheria  Zilizowekwa    Za Kufanya Maandamano  Kwani Wanaweza Sababisha  Matatizo Makubwa Nakwamba Walipaswa Kujadili  Kama Ajenda Na Kuziwasilisha Ofisi Ya Kata Ili Waweze Kusikilizwa .

 Kasinge Amesema   Kuwepo Na Walimu Saba  Hakuwezi Kuathiri Masomo Shuleni Na Kwamba Kuna Shule Nyingine Wilayani Humo Zina Walimu  Chache Kabisa Kuwanzia Watatu, Wanne  Huku Afisa Elimu  Wilaya Ya Wanging'ombe  Haruna Seremani  Akisema Mwalimu  Ambaye Wananchi Wanashinikiza Asihamishwe Amepangiwa Shule Ya Msingi Lyamluki.

Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Wanging'ombe   Amina  Kiwanuka  Amewataka Wananchi Kuyaweka Kwenye Maandishi Mawazo Yao   Ya Kuhitaji Walimu Ili Halmashauri Iweze Kuyashughulikia   Huku Akisema Maandamano Yao Yamekiuka Sheria  Na Kanuni Na Kusema Viongozi Wanatakiwa Kufanya Majadiliano Kabla Ya Kufanya Maandamano .


....................................................................................................................................................................................................

No comments:

Post a Comment