Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, August 30, 2016

MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WILAYA YA WANGING'OMBE HASSAN HABIBU JUMA YAFANYIKA JUMAPILI 28,2016

 HILI NI ENEO LA MAKABURI YA KIBENA ALIPOZIKWA MAREHEMU HASSAN HABIBU JUMA

 MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE ANTONY MAHWATA MWENYE SUTI NYEUSI KULIA NA ALIYEVAA MIWANI MKONO WA KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE  ALLY KASSINGE WAKIWA PAMOJA NA WANANCHI KWENYE MAZISHI YA MTUMISHI WAO.
 UMATI WA WANANCHI WA NJOMBE MJINI NA WILAYA YA WANGING'OMBE  WAKIWA MAKABURINI


 MWENYE BARAGASHIA NI IMAMU WA MSIKITI MKUU WA NJOMBE MJINI  RAJAB MSIGWA AKIONGEA NA UMATI MAKABURINI HAPO

 MUWAKILISHI WA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE JUMA CHALAMILA AMBAYE NI AFISA UTUMISHI WILAYA






 NI BAADA YA MAZISHI SASA WANANCHI NA VIONGOZI MBALIMBALI WANARUDI NYUMBANI KWA MAREHEMU BAADA YA  ZOEZI LA MAZISHI KUKAMILIKA


















Wananchi Mkoani Njombe Wametakiwa kuwasaidia watu wasiyo jiweza kwa kutoa misaada mbalimbali na kujenga tabia ya kuwatembelea wagonjwa na kuacha tabia ya kutumia uwezo wao wa mali walizonazo kuwanyanyasa wasiyojiweza waliopo karibu nao .

Rai hiyo imetolewa na Imamu wa msikiti Mkuu wa Njombe mjini Rajab Msigwa wakati wa mazishi ya aliyekuwa mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya  ya Wanging’ombe Hassan Habibu  Juma ambaye amefariki Augost 27 akiwa nyumbani kwake Nazareth.

Imamu Msigwa  ametumia fursa hiyo kuwaomba  wenye uwezo wa mali kusaidia makundi ya wasiyojiweza na wajane  huku wakiimarisha swala tano wakati wa uhai wao ili wasiulizwe na mwenyezi Mungu juu ya Neema ya mali walizokuwa nazo ambapo ameomba  waumini kusamehe waliowakosea na wao watasamehewa na Mungu.

Akisoma Historia ya marehemu Hassan Habibu Juma kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe ,Afisa utumishi Juma Chalamila  amesema marehemu alifariki ghafra kwa  ugonjwa wa presha akiwa nyumbani kwake baada ya kutoka Mkoani Mbeya alikokwenda kikakazi kabla ya kufariki.

Akizungumza  na waandishi mara baada ya mazishi ya marehemu Hassan Habibu Juma mwenyekiti wa Umoja wa madereva wa halmashuri Mkoa wa Njombe Patrick Mfikwa amesema kifo cha mwanachama mwenzao kimeacha pengo kubwa  kwa serikali na kwa umoja huo.


No comments:

Post a Comment