Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu
Kayandabila akiongea na watumishi wa Wizara ya Ardhi walioajiriwa hivi
karibuni wakati wa mafunzo ya awali kwa watumishi wa umma.
Baadhi
ya watumishi wa Wizara ya Ardhi walioajiriwa hivi karibuni
wakimsikiliza kwa makini Dkt. Yamungu Kayandabila wakati wa mafunzo ya
awali kwa watumishi wa umma.
Baadhi
ya Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
walipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi wakati wa mafunzo ya
awali kwa watumishi wa umma katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma
cha Magogoni jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila awataka watumishi
wa Sekta ya Ardhi kujiepusha na rushwa, kuzingatia kanuni na maadili ya
utumishi wa umma pamoja na kujiandaa kuhamia Dodoma.
Kayandabila aliyasema hayo wakati
akifungua mafunzo ya awali kwa watumishi wa umma walioajiriwa hivi
karibuni yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma cha
Magogoni jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment